AJALI:-Taswira ya Ajali ya Basi la Luhuye Express ikitokea April 21,2014,kijiji cha Itwimila wilayani Busega na kuua Watu 10 papo hapo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, April 22, 2014

AJALI:-Taswira ya Ajali ya Basi la Luhuye Express ikitokea April 21,2014,kijiji cha Itwimila wilayani Busega na kuua Watu 10 papo hapo.



Taarifa za awali zinaeleza kuwa basi hilo la kampuni ya Luhuye lililokuwa likitokea wilayani Tarime Mkoani Mara Kwenda Jijini Mwanza lilipata ajali April 21,2014 katika Kijiji cha Itwimila wilaya ya Busega Mkoani Simiyu , liliacha barabara na kugonga nyumba ambapo lilipinduka na kusababisha vifo vya watu 11 huku idadi kubwa ya abiria wakijeruhiwa vibaya.

Ajali hiyo iliyotokeoa April 21,2014,Majira ya kati ya saa nne na saa tano asubuhi,Miongoni mwa abiria waliokuwemo katika basi hilo ambao wamepoteza maisha ni Pamoja na Alex Masatu (Dj Alex da Wolf) ambae alikuwa ni mfanyakazi wa Radio Metro iliyoko Mkoani Mwanza…ambapo baadhi ya Majeruhi walikimbizwa katika hospital ya Wilaya ya Magu na wengine katika Hospital ya Rufaa Bugando kupatiwa matibabu.


Aidha watu 10 walikufa  papo hapo mmoja kufariki akiwa hospitali  na wengine 30 kujeruhiwa vibaya kufuatia ajali hiyo  mbaya ya Basi la Luhuye Express lenye namba za usajili T 410 AWT liliacha njia na  kugonga nyumba  ya Marehemu ,Mwalimu Lazaro Mbofu  na kuibomoa yote na kisha kupinduka.
Watu 10 wamekufa  papo hapo mmoja kufariki akiwa hospitali  na wengine 30 kujeruhiwa vibaya kufuatia  ajali mbaya ya Basi la Luhuye Express lililokuwa likitoka wilayani Tarime mkoani Mara kuelekea Jijini Mwanza.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa  kwa njia ya simu na Kamanda wa
Polisi mkoa wa Simiyu,Kamishina Mwandamizi wa Polisi(SACP)Charles
Mkumbo zinaeleza kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa 5:11 asubuhi
katika kijiji cha Itwimila wilayani Busega.

Alisema kuwa basi hilo lenye namba za usajili T 410 AWT liliacha njia
na  kugonga nyumba  ya Marehemu ,Mwalimu Lazaro Mbofu  na kuibomoa
yote na kisha kupinduka .

Kamanda Mkumbo alisema hadi sasa wametoa miili ya watu 10 katika basi
hilo na majeruhi zaidi 30 wamekimbizwa katika hospitali ya Rufaa ya
Bugando kwa matibabu zaidi.

“Hadi sasa kuna maiti 10 zilizopatikana eneo la tukio na zaidi ya watu
30 wamejeruhiwa na kukimbizwa katika hospitali ya Bugando kwa ajili ya
matibabu ila taarifa kamili nitaitoa baadaye juu ya watu waliokufa na
waliojeruhiwa kwani sasa nimetuma askari wa usalama barabarani
kufuatilia”alisema.

Mmoja wa mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo,Juma Ally mkazi wa kijiji
cha Itwimila akiongea na Mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu alisema kuwa
aliona basi hilo likiwa kasi na kupoteza mwelekeo na kutoka barabarani
na kisha kuigonga nyumba hiyo  na kuipita juu ya paa na kupinduka.

“Niliona Basi hilo lililokuwa likitokea barabara ya Musoma kuelekea
Mwanza likiwa katika mwendo wa kasi na dereva nadhani alishindwa
kulimudu na kasha kutoka nje ya barabara ya kuigonga nyumba na kisha
likapita juu ya nyumba hiyo na kisha kupinduka”alisema.

Na:- Simiyu yetu Blog


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad