Wananchi wawakiwa wanashuhudia ajali ya Basi la URIO iliotokea leo April 23,2014, jioni katika eneo
la KIA ambapo inasemekana watu zaidi ya 31 wamejeruliwa.
|
Picha chini na juu ni baadhi ya majeruhi walikuwa kwenye basi
hilo la Urio lililopata ajali leo April 23,2014,jioni katika eneo la Kia wilayani Hai
mkoani Kilimanjaro.
|
Basi aina ya Urio lenye namba za usajili T 137 BCX linalofanya
safari zake kutoka mjini Moshi kuelekea Leguruki mkoani Arusha leo(April
23, 2014) limepinduka katika eneo la KIA na kujeruhi watu zaidi ya 31.
Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo katika eneo la tukio walisema kuwa Dereva
wa basi hilo, alikuwa anajaribu kukwepa pikipiki iliyokuwa imejichomeka
barabarani.
"Dereva alikuwa anajaribu kukwepa pikipiki ndipo gari ikamshinda na
kuhama barabara, ndipo ilipo anguka gafla na kubiringita mara tatu hapa
yenyewe unavyoiyona tumeigeuza ilikuwa kichwa chini matairi juu"alisema
mmoja wapo wa shuhuda ambaye akutaka kutaja jina.
Habari Na:-Dj sek Blog.
No comments:
Post a Comment