Waandishi wa
Habari wakiwa jijini Mwanza kwenye Mafunzo Elekezi kwa Waandishi wa Habari wa
Gazeti la Mwananchi Kanda ya Ziwa leo March 16,2014.
|
Kutoka
kushoto ni Bw.Theophil Makunga na Bw.Midraji Ibrahimu(kulia) ambao ni Wahariri
wa Habari wa Gazeti la Mwananchi-Kanda ya Ziwa.
|
Wanahabari
wametakiwa kutumia uzalendo wa uhuru wa habari kwa kuepuka kuandika habari za
kushusha hadhi za watu pamoja a uchohezi na kusababisha uvunifu wa sheria
endapo hakutakuwa na ushahidi wa kutosha
kuhusu taarifa zao.
Meneja
utawala na sheria wa Mwananchi Communication Ltd Doris Maliale alisema hayo leo March 16,2014, katika mafunzo elekezi kwa wanahabari wagazeti hilo kanda ya ziwa na kwamba habari zenye migogoro
huleta hasara kwa Taasisi ama kampuni.
Alisema
madhara makubwa yanapotokea hukumba watumishi mbalimbali wa taasisi kuanzia mwandishi hadi mchapishaji
habari ambapo rasimali fedha hutumika na kuharibu mipango ya uzalishaji na
kuibua migogoro ndani ya jamii.
Alisema
katika kutumia maadili ya uandishi wajihadhari na kuwatishia watuhumiwa wa
mambo mbalimbali kwenye taasisi na lazima kukusanywe ushahidi wa pande mbili na
kujiridhisha na ukweli utakaokuwa umetolewa.
“Uandishi
unaweza kumpandisha mtu hadhi yake ama
kuishusha hivyo kunahitaji uangalifu katika kufanya kazi kwenye mazingira ya
habari ikiwa ni pamoja na kubainisha source husika kuliko kutaja kundi la watu
ama kampuni”.Alisema.
Kwa upande
wake mhariri mtendaji Theophil Makunga alisema kampuni ya MCL imekujipanua kwa
kuingia ubia na kampuni ya Jamana katika
kuchapa gazeti hilo na kusambaza nakala kwa wasomaji wengi kanda ya ziwa
ifikapo April mwaka huu.
Alisema
mpango wa kuanza kuchapicha nakala hizo tayari umekamilika kinachosubiliwa ni
Tanesco kusambaza umeme kwenye kiwanda cha uchapaji na magazeti
yatakayochapishwa ni mwananchi mwanaspoti na the Citzen.
“Tumejipanga
kuhudumia wananchi wetu kupata habari kwa wakati na mipango inapanuka mwaka
jana tulianzisha breacking news na tunatarajia hata kuwa na Tv na radio kufikia
mwakani na kuingia zaidi katika website”.Alisema Makunga.
Aidha mhariri
wa habari za kanda ya ziwa Midraji Ibrahimu alisisitiza wanahabari
kuhakikisha wanafika kwenye eneo la tukio na kutuma habari zenye uhakika ili jamii inawaamini na wao kufanya kazi katika
mazingira ya usalama.
Katika hatua
nyingine ,Kampuni ya gazeti la Mwananchi limepanua wigo wa kuandika habari
kutoka kanda ya ziwa kwa kutoa vipaumbele sita ili wananchi wapate habari
zinazoelezea changamoto na fursa katika sekta za uzalishaji mali.
Mhariri
mtendaji wa gazeti la Mwananchi Bw Bakari Machumu amesema hayo leo kwa
wanahabari walioko kanda ya ziwa wakati
wa semina elekezi juu ya mipango ya upanuzi na
utoaji huduma kwa wananchi wanaotakiwa kusoma gazeti hilo.
Bw Machumu
amesema kuwa katika habari za kanda ya ziwa kipaumbele ni katika sekta ya uchimbaji madini ,kilimo , uvuvi,siasa
,biashara na utalii pamoja na manufaa yake katika ujasiliamali ndani ya jumuia
ya afrika Mashariki.
Hata Hivyo
mhariri wa habari za kanda ya ziwa Midraji ibrahimu amesema Habari yoyote
itakayopelekwa mwananchi (MCL) lazima mwandishi awe amefika eneo la tukio na
kujiridhisha na mambo yanayotukia na kukusanya ushahidi wa kutosha.
Habari Na:-
Shaaban Ndyamukama
MWANZA.
No comments:
Post a Comment