|
Bidhaa hizo zimekamatwa
kufuatia ukaguzi uliofanywa na TFDA kwenye maduka 72 ya wilaya ya Kibondo na
mengine matano kwenye wilaya ya Kakonko.
|
|
Mamlaka ya Chakula na Dawa
TFDA kanda ya kati iliziteketeza bidhaa hizo bandia zilizokamatwa katika wilaya za Kibondo
na Kakonko Mkoani Kigoma.
|
Mamlaka ya
chakula na dawa TFDA Tanzania,Kanda ya kati imeteketeza tani moja na nusu
ya bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya
binadamu bidhaa ambazo zimekusanywa kutoka maduka mbali mbali yaliyoko katika
wilaya za Kakonko na Kibondo mkoani Kigoma.
Mkaguzi wa
chakula kutoka mamlaka ya chakula na dawa TFDA ,Kanda ya kati Bw. Abel
Deule amesema kuwa ofisi ya mamlaka ya
chakula na dawa TFDA kanda ya kati katika kutekeleza mpango kazi wake kwa robo
ya tatu ya mwaka wa fedha 2013/14 imefanya ukaguzi katika halmashauri za wilaya
ya Kibondo na Kakonko kwa kushirikiana na Ofisi za Waganga wakuu wa Halmashauri
hiz.
Amesema kuwa uelewa mdogo wa
wafanyabiashara kuhusu matakwa ya sheria ya chakula, dawa na vipodozi ndio
unaosababisha washindwe kufuatilia ubora na usalama wa bidhaa.
Aidha Bw Deule amesema kuwa
lengo la ukaguzi huo ni kuangalia hali ya usajili na vibali vya biashara, uwepo
wa bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu, usafi wa majengo na mpangilio wa
bidhaa pamoja na kuangalia uwepo wa dawa zilizofutiwa usajili.
Kwa upande
wake Afisa afya Mazingira wilayani Kibondo Bw.Joseph Kalobagwa amesema kuwa
elimu huotolewa kila wanapotembelea maduka mbali mbali ili kuhimiza kuacha tabia
ya kuagiza bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu.
Habari/Picha Na:-Kibondo Moto.
Habari/Picha Na:-Kibondo Moto.





No comments:
Post a Comment