Wanachama wa Simba SC wakiwa katika mkutano
huo uliofanyika asubuhi
ya leo March 16,2014,katika ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay
mjini Dar es Salaam.
|
Polisi
wakiwa tayari kumkabili mmoja wa wanachama aliyetaka kuleta zogo kwenye mkutano
huo.
|
Aliyekuwa
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' akitoa hoja.
|
Rage
akipongezwa na mmoja wawanachama wa Simba baada ya mkutano.
|
Wanachama wa Simba SC wakiwa katika mkutano
huo uliofanyika asubuhi
ya leo March 16,2014,katika ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay
mjini Dar es Salaam.
|
Rage
na Kaburu wakikumbatiana baada ya mkutano.
|
Rage
akipozi na Mwenyekiti wa zamani wa Simba SC, Hassan Dalali.
|
Rage
na Dalali wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa Simba SC.
|
WANACHAMA
wa Simba SC leo March 16,2014, wamepitisha marekebisho ya Katiba yao katika
mkutano uliofanyika kwenye Bwalo la Polisi, Oysterbay jijini Dar.
Mkutano
huo ulijumuisha wanachama wote hai wa klabu hiyo pamoja na uongozi wa juu wa
Simba wa Mwenyekiti, Ismael Aden Rage na kamati yake ya Utendaji.
Simba
imefanya marekebisho kwenye ibara ya 26(5 )sifa za wagombea ambapo kipengele
hicho awali kilikuwa kinasomeka “Asiwe aliyewahi kutiwa hatiani kwa kosa la
jinai kwa kuhukumiwa kifungo.
Kipengele hicho sasa kinasomeka “Asiwe ametiwa hatiani kwa kifungo cha zaidi ya miezi sita bila mbadala wa adhabu. Na endapo ametiwa hatihani kwa kifungo cha zaidi ya miezi sita, awe amemaliza muda wa miaka 5, tangu kuisha kwa kifungo husika bila kitiwa hatiana kwa jingine lolote la jinai.
Wanachama hao hao wamegoma kukipitisha ibara ya 26 (9) Mgombea awe ametimiza angalau miaka mitatu ya uanachama. Ambapo sasa kinasomeka angalau awe na mwaka mmoja wa wanachama.
Pia ibara ya 25 (8) (iii) wajumbe watano wa kamati ya utendaji. Mwenyekiti aruhusiwe kuteuwa wajumbe wengine watano wa kamati ya utendaji ambao anaweza kubadilisha kwa kadri anavyoona inafaa.
Wajumbe hawa wa kuteuliwa wanatakiwa
kuwa na sifa zilizile wanazotakiwa kuwa nazo wajumbe wa kuchaguliwa na
wanachama.
Baadhi ya vipengele vya katiba vilirekebishwa kwa kupigiwa kura na
wanachama huku vingine kupitishwa moja kwa moja kulingana na hoja zilizokuwa
zikitolewa mkutanoni hapo.
No comments:
Post a Comment