VPL 2013/2014:-Ripoti na matokeo ya mechi za Yanga vs Prisons – Azam FC vs Mgambo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, March 26, 2014

VPL 2013/2014:-Ripoti na matokeo ya mechi za Yanga vs Prisons – Azam FC vs Mgambo.



Vilabu vya Azam FC na Yanga SC leo  March 26,2014,wakabana koo katika mbio za ubingwa wa ligi kuu Vodacom  Tanzania bara baada ya vyote viwili kupata ushindi kwenye michezo yao waliyokuwa wakicheza kwa Azam FC ikiwa katika dimba la Mkwakwani ilikuwa ikicheza na Mgambo JKT na Kwa upande wa Yanga SC  walikuwa wakicheza na Tanzania Prisons kutoka Mbeya katika uwanja wa taifa.
Mabingwa Watetezi wa, Ligi Kuu Vodacom, Yanga SC, Leo March 26, 2014, hii Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam wameinyuka Tanzania Prisons Bao 5-0 .

Bao za Yanga SC zilifungwa na Emmanuel Okwi, Dakika ya 20, Mrisho Ngasa, Dakika ya 37, na mbili za Hamisi Kiiza, alieanzia Benchi na kufunga katika Dakika za 68 na 89, na Nadir Haroub "Cannavaro" kufunga Bao moja kwa Penati ya Dakika ya 79.

Nao Prisons walipata Penati katika Kipindi cha Kwanza baada ya Oscar Joshua kucheza Rafu lakini Mwangama alikosa.

Ushindi huo umewafanya Yanga wafikishe Pointi 46 kwa Mechi 21 na wako Nafasi ya Pili nyuma ya Azam FC waliocheza Mechi 22 na wana Pointi 50.

Mechi inayofuata kwa Yanga SC ni Jumapili huko Mkwakwani dhidi ya Mgambo JKT.

Katika mechi nyingine ya Ligi kuu ilikuwa ni Mgambo JKT dhidi ya Azam FC,ambapo bao za Kipindi cha Pili za John Bocco na Brian Umony zimewapa ushindi wa Bao 2-0 Azam FC walipocheza na Mgambo JKT huko Mkwakwani Jijini Tanga.

Matokeo haya yanawabakisha Azam FC kileleni wakiwa Pointi 4 mbele ya Yanga lakini Yanga wana Mechi 1 pungufu.

Jumapili Azam FC wana kibarua kigumu Jijini Dar es Salaam kwa kuivaa Simba SC.

VPL-LIGI KUU VODACOM 2013/2014.

Jumamosi Machi 29,2014.

Ashanti United v JKT Oljoro

Jumapili Machi 30,2014.

Mbeya City v Tanzania Prisons
Kagera Sugar v Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar v Coastal Union
JKT Ruvu v Rhino Rangers
Azam FC v Simba SC
Mgambo JKT v Yanga SC



MSIMAMO.

NA TIMU P W D L GD PTS
1 Azam FC 22 14 8 0 30 50
2 Yanga SC 21 13 7 1 27 46
3 Mbeya City 22 11 9 2 12 42
4 Simba SC 22 9 9 4 16 36
5 Kagera Sugar 21 8 8 5 3 32
6 Coastal Union 22 6 11 5 2 29
7 Ruvu Shooting 20 7 7 6 -4 28
8 Mtibwa Sugar 21 6 8 7 -1 26
9 JKT Ruvu 22 8 1 13 -15 25
10 Prisons FC 21 3 10 8 -9 19
11 Ashanti United 21 4 6 11 -18 18
12 Mgambo JKT 21 4 6 11 -19 18
13 JKT Oljoro 22 2 9 11 -17 15
14 Rhino Rangers 22 2 7 13 -17 13

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad