HISTORIA:-Kocha Pep Guardiola na Ubingwa wa Haraka Zaidi katika Ligi kuu soka Ujerumani. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, March 26, 2014

HISTORIA:-Kocha Pep Guardiola na Ubingwa wa Haraka Zaidi katika Ligi kuu soka Ujerumani.



Klabu ya FC Bayern München ya Ujerumani wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa 24 wa Bundesliga baada ya michezo 27 tu huku wakiwa na Mechi 7 mkononi baada ya kuifunga Ugenini Hertha Berlin Bao 3-1,- huu ndio ubingwa wa haraka zaidi katika historia ya Bundesliga.

Bao za Bayern katika Mechi hiyo ya Jana March 25, 2014,Usiku na Hertha Berlin zilifungwa na Toni Kroos, Dakika ya 6, Mario Goetze, Dakika ya 14, na Franck Ribery, Dakika ya 79 huku Bao la Hertha Berlin likifungwa kwa Penati ya Dakika ya 66 iliyopigwa na Adrian Ramos.

Ubingwa huu ni wa tatu kwa Pep Guardiola katika msimu wake wa kwanza, alishinda UEF Super Cup mwaka jana mwezi August, kisha wakashinda ubingwa wa klabu bingwa ya dunia December mwaka jana.

Je Guardiola ataweka rekodi ya kubeba makombe manne ndani ya msimu wake wa kwanza na Bayern Munich kwa kuchukua ubingwa wa klabu bingwa ya ulaya?

Huu ni Msimu wa kwanza wa Kocha wao Pep Guardiola ambae hajafungwa hata Mechi moja ya Bundesliga.

MSIMAMO-TIMU ZA JUU.

NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Bayern Munich 27 25 2 0 79 13 68 77
2 BV Borussia Dortmund 27 16 4 7 59 29 30 52
3 Schalke 04 27 15 6 6 51 37 14 51

Katika Mechi nyingine iliyochezwa Jana Usiku , Timu zilizo Nafasi za Pili na Tatu, Borussia Dortmund na Schalke 04 zilipambana na kutoka Sare ya 0-0.

REKODI:

-Bayern wamefunga si chini ya Bao 2 katika Mechi zao 18 zilizopita za Bundesliga, ambazo zote wameshinda, na hizo zote ni Rekodi.
-Bayern hawajafungwa katika Mechi 52 za Bundesliga na hii pia ni Rekodi.


BUNDESLIGA RATIBA/MATOKEO.

Jumanne Machi 25,2014.

BV Borussia Dortmund 0 Schalke 0
Hertha Berlin 1 Bayern Munich 3
SV Werder Bremen 1 VfL Wolfsburg 3
Eintr. Braunschweig 3 FSV Mainz 1

Jumatano Machi 26,2014.

Hamburger SV v SC Freiburg
FC Nuremberg v VfB Stuttgart
Eintracht Frankfurt v Borussia Mönchengladbach
TSG Hoffenheim v Hannover 96

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad