Azam
FC ambayo haijapoteza mechi yoyote msimu huu, imeonyesha kweli imejipanga baada
ya kutoa kipigo hicho kwa Simba ambayo mwaka huu imekuwa ikipepesuka, hivyo
kufikisha pointi 53 huku Yanga SC ikishika nafasi ya pili ikiwa na pointi 46.
Mechi
hiyo ya Azam FC iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, jana (March 30,2014) jijini
Dar es Salaam ilishuhudia Azam FC ikipata bao lake la kwanza kupitia kwa Hamis
Mcha katika dakika ya 16 baada ya mabeki wa Simba SC, Joseph Owino na Donald
Musoti kujichanganya.
Simba
SC ilisawazisha kupitia kwa Owino katika dakika ya 45 kwa kichwa kutokana na
mpira wa faulo uliopigwa na Wiliam Lucian.
John
Bocco ambaye alikuwa nje muda mrefu kutokana na majeraha, ameonyesha kurejea
kwa kasi baada ya kutupia bao la pili kwa Azam FC katika dakika 56 kutokana na shuti kali la
Kipre Tchetche kugonga mwamba na kurejea uwanjani.
Simba
SC ilionyesha kuamka katika dakika za mwisho za kipindi cha pili lakini bado mambo
yakawa magumu kwao.
Nao Mabingwa
watetezi wa Ligi kuu soka Vodacom Tanzania bara,Yanga SC sasa wapo hatarini
kuukosa Ubingwa wa Ligi- hiyo inafuatia Mbeya City kuilaza Prisons bao 1-0
jioni ya leo Uwanja wa Sokoine, Mbeya na kurejea rasmi kwenye mbio za ubingwa
wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Yanga SC baada ya kufungwa na Mgambo JKT mabao 2-1 Uwanja wa Mkwakwani, Tanga inabaki
na pointi zake 46 za mechi 22, wakati Azam FC ipo kileleni kwa pointi 53 za
mechi 23 baada ya kuifunga Simba SC mabao 2-1 Jana March 30,3014.
|
Matokeo mengine ya Ligi kuu Jana(March 30,3014), Kagera Sugar imelazimishwa sare ya bila kufungana na Ruvu Shooting, Mtibwa Sugar imeifunga mabao 3-1 Coastal Union na JKT Ruvu imeichapa 3-1 Rhino Rangers.
RATIBA YA
MECHI ZIJAZO LIGI KUU VODACOM TANZANIA 2013/2014.
Jumamosi
Aprili 5,2014.
Kagera Sugar
v Simba
Ashanti
United v Mbeya City
Jumapili
Aprili 6,2014.
Coastal
Union v Mgambo JKT
JKT Oljoro v
Tanzania Prisons
Rhino
Rangers v Mtibwa Sugar
Ruvu
Shooting v Azam FC
Yanga v JKT
Ruvu
Jumatano
Aprili 9,2014.
Yanga v
Kagera Sugar
**RATIBA
INAWEZA KUBADILIKA







No comments:
Post a Comment