MVUA:-Taswira ya Daraja linalounganisha Bagamoyo na Msata Lilivyofurika Maji (Machi 31, 2014) kufuatia Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali Nchini. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, March 31, 2014

MVUA:-Taswira ya Daraja linalounganisha Bagamoyo na Msata Lilivyofurika Maji (Machi 31, 2014) kufuatia Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali Nchini.

 Wakazi wa Kiwangwa, wakisaidiwa kuvushwa na vijana waliojitolea kujipatia ajira katika Daraja la Ruvu kwa kuwavusha Wananchi kwa kuwabea ama kuwaongoza njia ili kuvuka eneo hilo la daraja lililojaa maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini…ambapo Viajana hao wakiwavuja raia katika eneo hilo kwa ujila wa Sh. 2000 kwa kila aliyebebwa mgongoni asiyetaka kuvua viatu ama kugusa maji hayo, na Sh. 500 kwa kushikwa mkono kuongozwa njia kutoka mwanzo wa maji hayo hadi kuyavuka, na kuyaongoza magari kuvuka eneo hilo ni Sh. 3000 hadi 5000.

Kutokana na mvua kubwa iliyonyesha jana March 30,2014, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Bw.Ahmed Kipozi, alifika eneo hilo na kujionea wananchi wakitaabika kuvuka ene hilo na huku magari ya abiria yaliyokuwa yakitokea Bagamoyo kwenda Kiwangwa, yakibeba abiria na kuishia eneo hilo na kubeba wengine walioshushwa upande wa pili na kugeuza kwa kila abiria kulipa Sh. 1000. Na kisha abiria hao wakipata usafiri mwingine wa kubebwa na Vijana waliopo eneo hilo kwa Sh. 2000 kwa aliyependa ama 500 kwa kuongozwa njia.
 Haya ni baadhi ya madaraja ya barabara mpya inayojengwa yakiwa yamejaa maji.
Baadhi ya Vijana hao waliwavusha hadi wagonjwa katika eneo hilo kama anavyoonekana pichani akiwa amembeba mtu mzima anayeonekana kuwa ni mgonjwa.
Baadhi ya magari yaliyokaidi amri yakivuka eneo hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Bw.Ahmed Kipozi, akizungumza na madereva wa magari waliokuwa wakisubiri kuvuka eneo hilo pamoja na vijana waliokuwa wakitoa huduma ya kuwavusha watu.
Mkuu huyo wa Wilaya hiyo ametoa  tamko na kuwataka wakazi wa Kiwangwa kutokwenda Bagamoyo na wa Bagamoyo kutokwenda Kiwangwa, kwa kipindi chote cha mvua ili kuepuka maafa yanayoweza kutokea kwa kutumbukia na kusombwa na maji, ama daraja hilo la Jeshi kukatika kutokana na maji kuanza kupita juu ya daraja hilo jana (March 30,2014).
Haya ni baadhi ya maeneo hayo yaliyojaa maji, ambapo mmoja wa vijana hao anaonekana akipiga mbizi kwa furaha.
 'Bonge' la Mgahawa likiwa limejaa maji
Baadhi ya abiria walioshushwa upande wa pili wakiwania usafiri wa kuelekea Bagamoyo baada ya kufaulishwa na gari jingine la uapnde wa pili.
Dereva wa pikipiki akipakia gunia la mkaa vizuri ili awapakie na abiria wake wawili baada ya kuvuka darajani hapo.Picha Na:Sufiani Blog.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad