![]() |
|
Meneja wa
Chelsea Jose Mourinho akielekea jukwaani na alisirika na maamuzi ya mchezo na
kutoa maneno yasiyofaa kitendo ambacho kilimfanya Refa Chris Foy amtoe nje.
|
Hapo Jana
March 15,2014,Uwanja wa VILLA PARK, Chelsea, Vinara wa Ligi Kuu Uingereza,
wamekiona cha moto baada kufungwa 1-0 na Aston Villa na pia kumaliza Gemu
wakiwa Mtu 9 Uwanjani baada ya Kadi Nyekundu kwa Wachezaji wao wawili kutoka
Brazil, Willian na Ramires, na pia Meneja wao Jose Mourinho kutolewa nje na
Refa Chris Foy.
Balaa kwa
Chelsea lilianza Dakika ya 69 baada ya Willian kumwangusha Mchezaji Bora wa
Mechi hii, Fabian Delph, na kulambwa Kadi ya Njano ya Pili na kutolewa nje kwa
Kadi Nyekundu.
Katika
Dakika ya 82, Delph alikokota Mpira na kuwatambuka Wachezaji kadhaa wa Chelsea
na kumpasia kwenye Winga Mark Albrighton ambae alitoa krosi ya chini
iliyochezwa kwa kisigino na Delph na kufunga Bao zuri na la ajabu.
Huku Dakika
zikiyoyoma, Ramires wa Chelsea alipewa Kadi Nyekundu kwa kumkita El Ahmadi na
tukio hilo lilimfanya Meneja wa Chelsea Jose Mourinho akasirike na kutoa maneno
yasiyofaa kitendo ambacho kilimfanya Refa Chris Foy amtoe nje.
Chelsea bado
imebaki kileleni ikiwa Pointi 6 mbele ya Man City lakini wao wamecheza Mechi 3
zaidi ya Man City.
Matokeo
ya EPL 2013,2014 ,Jumamosi Machi 15,2014.
Hull 0 Man
City 2
Everton 2
Cardiff 1
Fulham 1
Newcastle 0
Southampton
4 Norwich 2
Stoke 3 West
Ham 1
Sunderland 0
Crystal Palace 0
Swansea 1
West Brom 2
Aston Villa
1 Chelsea 0
Ratiba ya Ligi kuu soka Uingereza (EPL) 2013,2014.
Jumapili
Machi 16,2014.
1630 Man
United v Liverpool
1900
Tottenham v Arsenal







No comments:
Post a Comment