![]() |
|
Baadhi ya magari yaliyokwama kupita baada ya
kufanyika kwa utekaji wa magari katika eneo la kijiji cha Kisaki manispaa ya
Singida.
|
Wakiongea na
waandishi wa habari, madereva ambao wamekutwa katika eneo hilo wameomba
jeshi la polisi kufanya doria mara kwa mara eneo hilo kwani kumekuwa na
matuki yanayo jirudia ya utekeji wa magari kwa kuweka mawe makubwa
barabarani na kuwajeruhi madereva jambo ambalo lina tishia amani kwa watumiaji
wa barabara.
Madereva wa
malori baada ya kufunga barabara naibu waziri wa Afrika mashariki Dr. Abdulla
Abdulla alikumbwa na adha hiyo na kusema ni haki ya kikatiba kwa madereva
kugoma kwa kudai haki zao, kutokana na hali hiyo amewahaidi madereva kupeleka
kilio chao katika mamlaka husika ili kuweza kutatua tatizo lao na kukomesha
vitendo vya uvamizi wa magari katika eneo hilo.
Kwa upande
wake kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida SACP Geofrey Kamwela
amesema madereva waliamua kusimama barabarani bila sababu yeyote kwa muda wa
zaidi ya masaa matatu na kusababisha foleni kubwa ambapo kwamujibu wa sheria za
usalama barabarani walikuwa wamefanya kosa ,lakini baada ya viongozi kufika na
kuwasikiliza waliamua kuendelea na safari.










No comments:
Post a Comment