![]() |
|
Basi la
Yanga SC limepata ajali likitokea mkoani Morogoro kwenda Dar es Salaam baada ya
mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar uliopigwa kwenye Uwanja wa
Jamhuri, Morogoro jana March 15,2014.
|
Katika ajali
hiyo iliyotokea majira ya saa tatu na nusu asubuhi ,Leo March 16,2014, hakuna
mtu yeyote aliyejeruhiwa na kwa sasa timu imeondoka na usafiri wa basi jingine
kuelekea jijini Dar es salaam.
|
Kikosi cha
Young Africans kilichoanza dhidi ya
Mtibwa Sugar,: 1.Kaseja, 2. Juma Abdul, 3.Oscar, 4. Cannavaro, 5. Yondani, 6.
Domayo, 7. Msuva, 8. Nizar/Dilunga, 9. Didier, 10. Okwi, 11. Kizza/Javu
|
|
Benchi la
Timu ya Soka ya Mtibwa ya Morogoro
Lilkiongzwa na Kocha wa Timu Hiyo
Meky Mexime Wa Kwanza Kushoto..
|
|
Mashabiki
waliojitokeza kwa Wingi Katika Uwanja w Jamhuri Mkaoni Morogoro Jana march 15,2014, Katika
Mchezo wa ligi kuu Kati ya Yanga Dhidi ya Mtibwa Sugar.
|
Aidha katika
mchezo wao wa Ligi Hapo Jana March 15,2014 ,Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu
ya Vodacom Tanzania bara timu ya Young Africans ilitoka suluhu (0-0 ) dhidi ya
timu ya Mtibwa Sugar ya Manugu katika mchezo uiofanyika kwenye dimba la Uwanja
wa Jamhuri mjini Morogoro.
Huko
Chamazi, Azam FC waliibamiza Coastal Union Bao 4-0 na kuendelea kujizatiti
kileleni. Bao za Azam FC zilifungwa na Kipre Tchetche, Bao 2, John Bocco na
Kevin Friday.
Azam FC
wamecheza Mechi 19 na wanaongoza Ligi wakiwa na Pointi 43 na kufuata Yanga SC
waliocheza Mechi 18 na wana Pointi 39.






No comments:
Post a Comment