Spika wa Bunge la 9 la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw Samuel Sitta awa Mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba-Tanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, March 12, 2014

Spika wa Bunge la 9 la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw Samuel Sitta awa Mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba-Tanzania.

Bw.Samuel Sitta ameshinda nafasi ya Mwenyekiti wa Bunge maalum la katiba kwa kura 487 na Bw.Hashim Rungwe kapata  kura 69 huku walio piga kura jumla ni Wabunge 566 ,kura zilizo halibika ni  kura 7.

Muonekano wa ukumbi wa bunge ambako Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wanakutana kujadili rasimu ya kanuni-Mjini Dodoma,Tanzania.
Wajumbe wa Bunge maalum la katiba wamemchagua Spika wa Bunge la 9 la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Bw Samuel Sitta kuwa Mwenyekiti wa bunge maalum la Katiba.

Katika uchaguzi huo uliofanyika leo jioni katika ukumbi wa Bunge hilo, Bw Sitta ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki alikuwa akichuana na Bw Hashim Rungwe ambaye aligombea Urais wa Tanzania mwaka 2010 kupitia NCCR Mageuzi kabla ya kuhamia CHAUMA.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo Mwenyekiti wa uchaguzi huo, amesema Bw Sitta ameshinda kiti hicho kwa kupata kura 487 ambapo Bw Hashim Rungwe amepata kura 69.

Aidha uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti utafanyika kesho March 13,2014, jioni, ambapo kufuatia Mwenyekiti kutokea Tanzania bara, Makamu Mwenyekiti atatakiwa kutokea Zanzbar kwa mujibu wa kanuni ambapo pia suala la Jinsia litazingatiwa.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad