SOMA TAARIFA YA (TMA):-Hali ya Hewa waonya uwapo wa kimbunga kitakachosababisha Mvua kubwa Nchini. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, March 31, 2014

SOMA TAARIFA YA (TMA):-Hali ya Hewa waonya uwapo wa kimbunga kitakachosababisha Mvua kubwa Nchini.


Mvua za masika zinazoendelea kunyesha nchini zimeendelea kuleta maafua ambapo Daraja linalounganisha Bagamoyo na Msata limefurika asubuhi ya kuamkia leo (Machi 31, 2014)…ambapo Mkuu wa Wilaya ya Bayamoyo,Bw. Ahmed Kipozi ameiambia FikraPevu kuwa ofisi yake imewataka wasafiri kutoitumia barabara hiyo ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kutokea.
Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imetahadharisha juu ya kuwapo kwa kimbunga kiitwacho Hellen katika mwambao wa Bahari ya Hindi ambacho kitasababisha mvua kubwa inayozidi mililita 50 ndani ya saa 24 kuanzia jana March 30,2014, katika mikoa 14 nchini.

Taarifa ya mamlaka hiyo ambayo imetolewa jana (March 30,2014) kwa vyombo vya habari imebainisha kuwa mvua zitanyesha katika mikoa ya Dar es Salaam, Mtara, Lindi, Tanga, Unguja, Pemba, Singioda, Dodoma, Ruvuma, Katavi, Njombe, Mbeya na Morogoro.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa mvua hizo zilitarajia kuanzia jana na zitaendelea hadi Aprili Mosi mwaka huu na wakazi wa mikoa hiyo, watumiaji wa bahari pamoja na mamlaka zinazohusika na maafa zimetakiwa kuchukua tahahadhari zinazotakiwa.

Imebainisha kuwa, uwezekano wa mvua hizo ni asilimia 80 na ni mwendelezo wa mvua za masika zinazoendelea kunyesha nchi nzima katika baadhi ya maeneo ambako hupata misimu miwili ya mvua kwa mwaka.

“Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia na itatoa taarifa zaidi kadri zitakavyopatikana,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo na kuongeza kuwa, uangalifu na tahadhari vinahitajika ili kuepusha maafa zaidi.

Kimbunga hicho kinakuja wakati baadhi ya maeneo nchini, wiki iliyopita zilikumbwa na mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali sasa na kusababisha uharibifu wa mali na miundombinu. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad