BINGWA WA MATAJI:- Bondia Mashali amshinda Japhet Kaseba,Ngumi zilipigwa haswaaaa……..’’ - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, March 30, 2014

BINGWA WA MATAJI:- Bondia Mashali amshinda Japhet Kaseba,Ngumi zilipigwa haswaaaa……..’’


Bondia Mashali, akipozi na mikanda yake baada ya kukabidhiwa mkanda mmoja Jana March 29,2014,Usiku  baada ya kufanikiwa kutwaa taji la WBO uzito wa Light kwa Pointi 97-93.


Bondia Thomas Mashali (kushoto) akikwepa konde la Japhet Kaseba, wakati wa pambano lao kuwania Ubingwa wa WBO uliofanyika kwenye ukumbi wa UBO Africa Mashali.  Sabasaba jijini Dar es Salaam. Katika pambano hilo Mashali alimshinda mpinzani wake kwa Pointi. 


Mabondia Japhert Kaseba (Thomas Mashali) wakipambana wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba kugombania ubingwa wa UBO Africa Mashali. Mashali alishinda kwa Pointi.


Japhet Kaseba (kushoto) akiwa na mpinzani wake, Japhet Kaseba,Pamoja na ushindi, lakini Mashali hakucheza katika kiwango chake kiasi cha kumaliza raundi 10 na rasta mwenzake huyo lakini Japhet aliridhia uamuzi wa majaji na kumkumbatia Mashali baada ya pambano.

Bondia Thomas Mashali amefanikiwa kutwaa taji la WBO uzito wa Light Heavy baada ya kumshinda kwa pointi Japhet Kaseba Jana March 29,2014,usiku kwenye ukumbi wa PTA, Sabasaba, Temeke mjini Dar es Salaam.

Majaji wote watatu walimpa ushindi bondia wa Manzese wa pointi 97-93 dhidi ya mbabe wa Kinondoni baada ya pambano hilo la raundi la 10, ambalo lilimalizika bila mtu kuanguka chini hata kwa sekunde wala kuhesabiwa kwa kuleweshwa ngumi.

Kaseba alifanya vizuri katika raundi ya saba na ya nane, lakini Mashali akazinduka raundi ya tisa na kumalizia ya 10 pia vizuri. 

Japokuwa hata matokeo yangetangazwa sare kusingekuwa na malalamiko, lakini Japhet aliridhia uamuzi wa majaji na kumkumbatia Mashali baada ya pambano.

Katika mapambano ya utangulizi, Alan Kamote alimshinda kwa Technical Knockout (TKO) raundi ya tano Karage Suba na kutwaa ubingwa wa UBO uzito wa Light, pambano kati ya Freddy Sayuni na Rajab Maoja lilivunjika raundi ya nne baada ya Maoja kuchanika na kushindwa kuendelea kugombea ubingwa wa PST. 

Said Mundi alimpiga Jumanne Mohamed kwa pointi pambano la uzito wa bantam, Issa Nampepeche alimpiga kwa pointi Zuberi Kitandula uzito wa bantam pambano lisilo la ubingwa, Saidi Chaku alitoka sare na Jocky Hamisi pambano la Feather lisilo la ubingwa na Majid Said alimpiga kwa pointi Frank Zaga uzito wa bantam pambano lisilo la ubingwa pia. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad