Hayo ndiyo
yaliyokikuta kikosi cha mashetani wekundu, Manchester United baada ya kupokea
vibano mfululizo kutoka kwa timu pinzani, hali iliyosababisha mashabiki wake
wapatao 450,000 kujiondoa(Unlike) katika page ya timu hiyo kwenye mtandao wa
Facebook baada ya kukatishwa tamaa kwa kukubali kufungwa dimbani kwao
‘Old Trafford’ jumla ya mabao 0 -3 dhidi ya Mahasimu wao wakubwa
Liverpool kwenye Ligi Kuu England na kuwaacha wakiwa Pointi 18 nyuma ya Vinara
Chelsea na hivyo kuwa kwenye hali isiowezekana kutetea tena Taji lao la Ubingwa
Msimu huu 2013/2014.
Pamoja na
hayo Meneja wa Man United ,DAVID MOYES amesisitiza kwamba ana uhakika nafasi
yake kama Meneja wa Manchester United haina wasiwasi licha ya Klabu hiyo
kusuasua katika Msimu wake wa kwanza na Magazeti kadhaa huko Uingereza kutabiri
kufukuzwa kwake.
Pia, Msimu
huu, katika Mechi 14 za Ligi walizocheza kwao Old Trafford, Man United
wamefungwa Mechi 6 kati ya 14.
Wakiwa
wanakabiliwa na Mechi ya Marudiano ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na Olympiakos ya
Ugiriki Jumatano March 19, 2014,Usiku ambayo wanatakiwa kupindua kipigo cha Bao
2-0 ili wao wasonge mbele, Moyes, akihojiwa na Wanahabari ikiwa kushindwa
kuitoa Olympiakos kutaathiri hatima yake Man United, alijibu: “Hatima yangu
haijabadilika hata chembe! Nina kazi nzuri! Najua mwelekeo upi nakwenda!”
Inaaminika
Bodi ya Man United, kwa sasa, haifikirii kumbadili David Moyes licha ya kufanya
vibaya mno wakiwa Nafasi ya 7 kwenye Ligi huku wakibakiwa na Mechi 7.
Akizungumza
na Wanahabari kwenye Mahojiano hii Leo, Moyes amesema ana sapoti kubwa ya
Viongozi wa Man United akiwemo Sir Alex Ferguson ambae ndie amemrithi.
Moyes
aliongeza: “Hii ni Klabu ambayo Dira yake ni ya muda mrefu, si muda mfupi na
ndio maana nimepewa Mkataba wa Miaka 6!”
Hii Leo March
18, 2014, huko Uingereza, Magazeti yalipambwa na habari kuwa Moyes amepewa Siku
10 za kufanya vizuri ambapo watakuwa na Mechi 3, dhidi ya Olympiakos, West Ham
na Man City, la sivyo kibarua hana.






No comments:
Post a Comment