Basi la Taqwa lapata Ajali leo na kujeruhi Abiria kadhaa, likitokea Dar es Salaam kuja Ngara –Bujumbura. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, March 18, 2014

Basi la Taqwa lapata Ajali leo na kujeruhi Abiria kadhaa, likitokea Dar es Salaam kuja Ngara –Bujumbura.


Chumba cha blog hii kupitia Whatsapp , kimearifiwa na kutumiwa picha za tukio la ajali eneo la Daraja la mto Ruvu barabara kuu ya Dar es salaam-Morogoro na Mdau Elisante, akitufahamisha kutokea kwa Ajali ya Basi la Taqwa leo Asubuhi, lililokuwa limetoka Leo March 18, 2014,Dar es salaam kupita wilayani Ngara mkoani Kagera, kesho March 19, 2014,Asubuhi kwenda Jijini Bujumbura nchini Burundi kupata ajali ambapo katika tukio hilo abiria kadhaa wamejeruhiwa.

Kulingana na mashuhuda wa tukio hilo, wamebainisha kuwa athari ya ajali hiyo imesababishwa na basi lingine kulipita basi la taqwa ,kisha likiwa mwendo kasi kukutana na magari mengine mbele yake, hivyo Dereva wa basi la Taqwa kutaka kutanua zaidi ndipo lilipomshinda na kupinduka.

Blog ya Mwanawamakonda tunatoa pole kwa Majeruhi na tunawaombea wapone haraka majeraha yao’’AMINA.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad