LA LIGA 2013/2014:-Haya ndio Matokeo ya Atletico Madrid, FC Barcelona na Real Madrid wakishinda Mechi zao na kuzidi kukabana koo kileleni. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, March 30, 2014

LA LIGA 2013/2014:-Haya ndio Matokeo ya Atletico Madrid, FC Barcelona na Real Madrid wakishinda Mechi zao na kuzidi kukabana koo kileleni.


Lionel Messi akishangilia baada ya kufunga bao pekee katika ushindi wa Barcelona wa 1-0 dhidi ya jirani zao Espanyol.
Mshambuliaji Messi amevunja mwiko wa kutowafunga Espanyol kwenye Uwanja wao wa Cornella El Prat baada ya Jana March 29,2014, kuifungia bao pekee FC Barcelona dhidi ya wenyeji wao hao.

Messi hakuwahi kufunga katika Uwanja huo katika misimu mitano, lakini jana hakufanya makosa alipokwenda kupiga penalti baada ya beki wa pembeni, Javi Lopez kuunawa mpira kwenye eneo la hatari.

Barcelona sasa inafikisha pointi 75 baada ya mechi 31 na inaendelea kukaa nafasi ya pili nyuma ya Atletico Madrid yenye pointi moja zaidi, baada kuifunga Athletic Club 2-1.



Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia Real bao lake la 28 katika msimu huu wa La Liga.

Nae nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo na Gareth Bale walirejesha urafiki wao tena wakati timu yao ikiifumua mabao 5-0 Rayo Vallecano Jana March 29,2014,usiku  katika mchezo wa La Liga uliofanyika Uwanja wa Santiago Bernabeu.

Bale alimsetia Ronaldo kuifungia Real Madrid bao la kwanza dakika ya 14, na akachangia bao la pili lililofungwa na Carvajal dakika ya 54, kabla ya kufunga la tatu dakika ya 67 na la nne dakika ya 70 wakati Morata alifunga la tano dakika ya 77. 

Real sasa inatimiza pointi 73 baada ya mechi 31, lakini inaendelea kuketi nafasi ya tatu nyuma ya FC Barcelona yenye pointi 75 na Atletico Madrid pointi 76 kileleni, zote zikiwa zimecheza mechi 31 pia.

Ronaldo alimkasirikia Bale baada ya kwenda kupiga mpira wa ovyo dakika za mwishoni Real ikilala 4-3 mbele ya Barcelona wiki iliyopita, lakini jana amemaliza hasira za mchezaji mwenzake huyo na kurudisha urafiki wao tena.

Position Team Played Goal Difference Points
1 Atlético Madrid 31 47 76
2 Barcelona 31 64 75
3 Real Madrid 31 54 73
4 Athletic Bilbao 31 19 56
5 Sevilla 31 9 50
6 Real Sociedad 30 10 49
7 Villarreal 30 14 48
8 Espanyol 31 -2 40
9 Valencia CF 30 1 40
10 Levante 30 -11 37
11 Celta de Vigo 31 -10 36
12 Granada CF 30 -12 34
13 Rayo Vallecano 31 -34 33
14 Málaga 30 -9 32
15 Elche 30 -17 31
16 Almería 30 -24 30
17 Osasuna 30 -26 29
18 Getafe 30 -21 28
19 Real Valladolid 30 -19 27
20 Real Betis 30 -33 22

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad