![]() |
|
Mchezaji wa
Crystal Palace, Jason Puncheon (kushoto) akishangilia huku Terry akisigina
kichwa chake chini baada ya kujifunga na kuipa ushindi wa bao 1-0 Crystal
Palace.
|
![]() |
|
Wachezaji wa
Crystal Palace wakishangilia ushindi wao wa leo dhidi ya Chelsea.
|
Matumaini ya
Chelsea kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Uingereza yameingia dosari kubwa leo March 29,2014,baada
kuchapwa Bao 1-0 na Crystal Palace, Timu ambayo inapigana kujinusuru na kubakia
kwenye Ligi hiyo, katika Mechi iliyochezwa Uwanja wa Selhurst Park.
Bao hilo la
ushindi kwa Palace lilifungwa na Nahodha wa Chelsea, John Terry, baada kupiga
Kichwa wavuni kwao wenyewe kufuatia Krosi ya Dakika ya 52 ya Joel Ward.
Mara mbili
Kipa wa Palace, Julian Speroni, aliokoa toka kwa Eden Hazrd na pia John Terry
alipata nafasi safi lakini Kichwa chake kilipaa.
Palace
walikaribia kupata Bao la Pili lakini Shuti la Cameron Jerome lilipiga Posti.
Huo ni
mchezo wa pili mfululizo The Blues wanafungwa ugenini, baada ya awali kufungwa
na Aston Villa na sasa inabaki na pointi zake 69 za mechi 32 mbele ya Liverpool
yenye 68 za moja 31.
![]() |
|
Rooney
akifunga kwa penati na kuipa Mabao mawili Manchester United katika dakika za 20
na 45 na mengine ya Juan Mata dakika ya 57 na Javier Hernandez dakika ya 90
yalitosha kuiongezea pointi United.
|
![]() |
|
Juan Mata
akipambana na Bacuna na furaha kwa kocha David Moyes kufuatia Manchester
United kuifunga mabao 4-1 Aston Villa Uwanja wa Old Trafford March 29, 2014,katika
mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza.
|
Mabingwa wa Uingereza,
Manchester United, wakicheza kwao Old Trafford Leo March 29, 2014, wamepata Mechi nzuri ya
kupasha moto kabla Jumanne hawajawavaa Mabingwa wa Ulaya, Bayern Munich,
katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI itakayochezwa
Uwanjani hapo hapo baada ya kuitandika Aston Villa Bao 4-1 katika Mechi ya Ligi
Kuu Uingereza.
Aston Villa
ndio waliotangulia kupata Bao kati Dakika ya 13 baada ya Frikiki ya Westwood
kumshinda nguvu Kipa De Gea lakini Wayne Rooney akaifungia Man United Bao 2
moja likiwa Penati iliyotolewa baada ya Juan Mata kuangushwa ndani ya Boksi.
Juan Mata
aliongeza Bao la Tatu katika Kipindi cha Pili na hilo ni Bao lake la Kwanza
tangu ahamie Man United Mwezi Januari kutoka Chelsea.
Bao la 4
lilifungwa na Chicharito, alietokea Benchi, baada ya kazi nzuri ya Adnan
Januzaj ambae nae pia aliingizwa Kipindi cha Pili.
Kabla Mechi
hii kuanza Washabiki wa Manchester United walionyesha sapoti yao kwa Meneja wao
David Moyes kwa kumshangilia wakati akiingia Uwanjani kwenda kukaa kwenye
Benchi kabla Mechi kuanza na kuizomeoa ile Ndege iliyopita juu ya Anga ya Old
Trafford ikiburuza Bango kubwa: 'Wrong One - Moyes Out' wakati Mechi imeanza
tu.
Mashabiki,
hasa wale waliokwaa Jukwaa maarufu la Old Trafford liitwalo Stretford End,
waliimba na kumshangilia Moyes: “One David Moyes!”.
MATOKEO YA MECHI
LIGI
KUU UINGEREZA.
Man Utd 4 - 1 Aston Villa
Crystal Palace 1 - 0 Chelsea
Southampton 4 - 0 Newcastle
Stoke 1 - 0 Hull
Swansea 3 - 0 Norwich
West Brom 3 - 3 Cardiff
Arsenal 1 - 1 Man City
RATIBA
LIGI
KUU UINGEREZA.
Jumapili
Machi 30,2014.
1530
Fulham v Everton
1800
Liverpool v Tottenham
Jumatatu
Machi 31,2014.
2200 Sunderland v West Ham
| Position | Team | Played | Goal Difference | Points |
|---|---|---|---|---|
| 1 | Chelsea | 32 | 38 | 69 |
| 2 | Liverpool | 31 | 45 | 68 |
| 3 | Man City | 30 | 52 | 67 |
| 4 | Arsenal | 32 | 19 | 64 |
| 5 | Everton | 30 | 16 | 57 |
| 6 | Tottenham | 31 | 0 | 56 |
| 7 | Man Utd | 32 | 14 | 54 |
| 8 | Southampton | 32 | 9 | 48 |
| 9 | Newcastle | 32 | -9 | 46 |
| 10 | Stoke | 32 | -8 | 40 |
| 11 | West Ham | 31 | -7 | 34 |
| 12 | Aston Villa | 31 | -12 | 34 |
| 13 | Swansea | 32 | -3 | 33 |
| 14 | Hull | 32 | -7 | 33 |
| 15 | Norwich | 32 | -25 | 32 |
| 16 | Crystal Palace | 31 | -19 | 31 |
| 17 | West Brom | 31 | -12 | 29 |
| 18 | Cardiff | 32 | -32 | 26 |
| 19 | Sunderland | 29 | -19 | 25 |
| 20 | Fulham | 31 | -40 | 24 |










No comments:
Post a Comment