Tazama Taswira ya hitimisho la Kampeni za M4C Pamoja Daima za CHADEMA lililofanyika jana katika uwanja wa Furahisha Mwanza. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, February 02, 2014

Tazama Taswira ya hitimisho la Kampeni za M4C Pamoja Daima za CHADEMA lililofanyika jana katika uwanja wa Furahisha Mwanza.

Wananchi wa Jiji la Mwanza wakiwa wamekaa kwa utulivu katika Mkutano wa hitimisho la Chadema M4C Pamoja Daima ulifanyika katika Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza Jioni ya Jana (Februari 01,2014).

Chopa iliyokuwa imembeba Katibu Mkuu wa Chadema Dr. Wilbroad Slaa ikitua katika Uwanja wa Furahisha ili aweze kuhutubia katika Mkutano wa Kampeni wa Chadema M4C Pamoja Daima.

Wananchi wa Jiji la Mwanza wameinua mikono ishara ya Kusurrender katika Mkutano wa hitimisho a Chadema M4C Pamoja Daima ulifanyika katika Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza Jioni ya Jana (Februari 01,2014).

Ze nyomiziiiiiii ndani ya uwanjaa wa Furahishaaa wakisikiliza hotuba mbalimbali kutoka kwa viongozi wa Chadema walioko kwenye Kampeni ya M4C Pamoja Daimaa.

Mbunge wa Nyamagana Mheshimiwa Ezekia Wenje akiwa na Matibu wa Chadema Taifa Bwan Mudi mwenye kombati ya Green na Mbungue wa Jimbo la Ilemela Mheshimiwa Highness Kiwia.



Mheshimiwa Higness Kiwia akimpokea Bwana Darius Ngoko ambaye ameamua kuhama chama cha Mapinduzi CCM na Kujiunga na Chadema katika Mkutano wa M4C Pamoja Daima.

Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasiana Maendeleo Chadema Bwana Wilfred Mganyizi Lwakatare akitoa speecha yake ya kusalimia Mkutano wa M4C Pamoja Daima katika viwanja vya Furahisha.



Katika hali ya kushangaza jeneza ambalo lilikuwa limechorwa picha ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zitto Kabwe nalo lilionekana mbele ya Kamera kama inavyoonekana.

Katibu wa Chadema Taifa Dr. Wilbroad Slaaa akihuthubia maelfu ya watanzania waliofurika katika uwanja wa Furahisha Mwanza kusikiliza hitimisho la Kampeni ya M4C Pamoja Daima jana Februari 01,2014.

Ze nyomiziiiiiii ndani ya uwanjaa wa Furahishaaa wakisikiliza hotuba mbalimbali kutoka kwa viongozi wa Chadema walioko kwenye Kampeni ya M4C Pamoja Daimaa.


Pamoja na mambo mengine katika mkutano huo,Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimesema hakitalalamika tena kwa lolote au kukilamu Chama Cha Mapinduzi CCM maana wameshaongea sana na sasa watafanya utekelezaji wa Ilani ya Chama chao.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Chama hicho Dr. Wilbroad Slaa katika hitimisho la Kampeni za M4C Pamoja Daima lililofanyika jana Februari 01,2014 katika uwanja wa Furahisha Mwanza.

Dr. Slaa amesema kuwa wameshaongea kero mbalimbali za wananchi wa Tanzania lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyika hivyo wao kuanzia sasa wao kama Chadema hawatalalamika zaidi ya kuchukua maamuzi ya utekelezaji tu.

Kampeni hizo ambazo zimefanyika kwa siku 14 kwa kutembelea Majimbo yote ya upigaji kura ambayo yalikua yamegawanyika katika makundi mawili kwa kutumia chopa tatu ambazo zilikuwa zinaongozwa na Dr. Wilbroad Slaa, Freeman Mbowe na Tundu Lissu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad