Matokeo hayo
ni nafuu kwa Chelsea hasa baada ya Klabu zote za Uingereza zinazoshiriki UEFA
msimu huu, Arsenal, Manchester City na Manchester United, zote kupigwa Bao 2-0
kwenye mchezo wa kwanza 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Chelsea
walitangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya 9 la Fernando Torres huku Katika
Dakika ya 54, Galatasaray walisawazisha baada ya Kona ya Wesley Sneijder
kukoswa na Jerry Terry na Aurelien Chedjou kuunganisha wavuni.
Wakicheza
Ugenini huko Veltins Arena Jijini Gelsenkirchen Nchini Ujerumani, Real Madrid
walishinda Mechi hiyo ya Kwanza ya UEFA kwa kuichapa Schalke Bao 6-1 kwa bao za
Gareth Bale,Cristiano Ronaldo , Benzema kwa kila mmoja kufunga mawili.
Schalke
walifunga Bao lao pekee katika Dakika ya 90 Mfungaji akiwa Klaas-Jan Huntelaar.
UEFA CHAMPIONZ LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16 Bora.
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza]
[Saa za Bongo]
Jumanne Machi 11,2014.
22:45 Bayern Munich v Arsenal FC [2-0]
22:45 Atletico de Madrid v AC Milan [1-0]
Jumatano Machi 12 ,2014.
22:45 FC Barcelona v Manchester City [2-0]
22:45 Paris Saint-Germain v Bayer 04 Leverkusen [4-0]
Jumanne Machi 18,2014.
22:45 Chelsea FC v Galatasaray Spor Kulübü [1-1]
22:45 Real Madrid CF v Schalke 04 [1-6]
Jumatano Machi 19 ,2014.
22:45 BV Borussia Dortmund v Zenit St. Petersburg [4-2]
22:45 Manchester United v Olympiacos CFP [0-2]
No comments:
Post a Comment