KCC ya Uganda Bingwa wa Kombe la Mapinduzi 2014, baada ya kuilaza Simba SC 1-0 . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, January 13, 2014

KCC ya Uganda Bingwa wa Kombe la Mapinduzi 2014, baada ya kuilaza Simba SC 1-0 .


Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein kushoto akimkabidhi Kombe la ubingwa wa Mapinduzi, Nahodha wa KCC ya Uganda, Fahad Kawooya jioni ya leoari 13,2014) Uwanja wa Amaan, baada ya kuifunga Simba SC 1-0.

KCC ya Uganda leo(Januari 13,2014) huko Amaan Stadium, Zanzibar wametwaa Mapinduzi Cup, moja ya Sherehe mahsusi kusheherekea Miaka 50 ya Mapinduzi matukufu, baada kuitungua Simba Bao 1-0.

Shujaa wa KCC ni Herman Wasswa aliefunga Bao pekee la Fainali hii katika Dakika ya 20 baada kupokea Krosi kutoka Habib Kavuma na kumtambuka Beki Mkenya Donald Musoti na kumchambua Kipa Ivo Mapunda.

Hii ni mara ya pili kwa KCC na Simba kukutana kwenye michuano hiyo baada kutoka 0-0 katika hatua za Makundi na hii ni mara ya kwanza kwa Simba, inayofundishwa na Kocha toka Serbia Zdravko Logarusic, ‘kutobolewa’ kwa Bao katika Mashindano hayo.

Mbali ya kunyakua Kombe, KCC pia wamezoa zawadi ya Dola 10,000 kama Mabingwa.

Kwenye Ufungaji Bora, Kiungo wa URA, Owen Kasule, alitwaa Tuzo ya Ufungaji Bora akiwa na Bao 4 na Herman Wasswa, wa KCC, na Amri Kiemba, wa Simba, wanafuatia wakiwa na Bao 3.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad