Mapenzi
na kufanya mapenzi baina ya wawili wapendanao hasa kama wameoana ni moja ya chachu ya ndoa ambayo
husaidia kushikilia na kuimarisha ndoa hiyo endapo ikatumika vizuri na kwa wote
kufurahia hasa kwa wale ambao hushirikiana katika kila kitu.
Siri ya
kufurahia tendo la ndoa ni wanandoa wote kuridhika na utendaji wa mwenza wao hasa wakati wa
tukio, kwa kujituma, kuwa mbunifu, kutaka na kufurahia tendo hilo.
Ingawa ni
kweli kwa nadra inaweza tokea mwenzako akawa na hamu na wewe usiwe nayo
(ikitokea mara chache sana – hili linaeleweka, na linaweza kukubalika ila si
kwa kuzoea na ikawa utamaduni; iwe kwa mwanaume ama mwanamke).
Izingatiwe
kuwa, kufurahia tendo la ndoa haiji kirahisi rahisi… Mazingira ya kufurahia tendo hili
muhimu ni lazima yajengwe na yaimarishwe mara kwa mara.
Maana ni wazi kuwa uhai
wa kila ambalo linatakiwa kuishi ni lazima litunzwe kwa umakini na kujali.
Hivyo kufurahia tendo la ndoa pia hupaswa kuimarishwa kwa nilivyotaja hapo
awali – Kupenda, kujituma, utundu, maarifa na Ubunifu.
Na haya yote huwa rahisi
sana ikiwa mwanandoa wako wampenda ama kumkubali, na kubwa kuliko ikiwa na yeye
pia hujituma, ‘ni mtundu’ na ana maarifa pia.
Hivi vitu
(Kujituma, utundu, maarifa na ubunifu) haviji hivi hivi pia… Na ndio kwa misingi hiyo wanandoa
hushauriwa kuzungumzia tendo la ndoa, kama haridhiki katika tendo, kitu kipi
hupendi, kitu gani unapenda, wapi unapenda kuguswa, vipi unapenda kukunwa,
na ni kitu gani ambacho kinakupandisha mzuka – huku wewe mwenzie ukiwa
mtundu katika kuhakikisha unavumbua maeneo mengine ambayo hata yeye hakujua
kuwa anaweza pata raha hiyo ambayo anaipata kwa wakati huo (TAHADHARI – Yapaswa
kuwa na mipaka pia).
Mnaweza
msiwe kila mmoja si mtaalam kwa mwenzie mnapoanza mahusiano yenu ya mapenzi, ila inapaswa na ni
jukumu la kila mmoja kuhakikisha ufundi huo unaongezeka kadri siku zinavyozidi
kwenda kwa mwenza wake huyo na si kupungua.
Izingatiwe pia kuwa, Kufanya
mapenzi si lazima ukafanya kama vile ambavyo picha za ngono huonyesha ili kujua
mnafurahia, msingi ni kutafuta rhyme ambayo huwafanya wote mfurahie
tendo hilo la ndoa na kuwafanya kuwa na kiu juu ya mwenza wako pale unapokuwa
umemkosa.
Ndoa si
kufanya tu Mapenzi ni zaidi ya hapo, ila mwisho wa siku kufanya Mapenzi ni muhimu mno kwa ustawi
wa ndoa kati ya wanandoa.
Ni suala ambalo kiharaka haraka linaweza chukuliwa
kwa wepesi, ila mwisho wa siku lina faida sana.
FAIDA YA
TENDO LA NDOA KWA WANANDOA
Linajenga
ukaribu zaidi kwa wanandoa.
Tokana na
majukumu ya kifamilia ambayo yanaenda yakikua kwa kasi na kufanya baadhi ya
wanandoa kutokuwa na wakati wa kuwa karibu zaidi kunakuwa na muda mchache kwa
baadhi kubadilishana mawazo.
Wanandoa wengine wamefaulu kwa kuhakikisha kila
siku/au mara kadhaa kwa juma kujulishana habari zao wanapokuwa hawapo pamoja.
Tendo la ndoa linaweza tumika kama wakati muafaka wa kila mmoja kutiririka na
kuongea mambo mbalimbali na hata kupanga mipango yenu ya kimaisha.
Hilo hutokea
pale mnapokuwa mnataka kujianda, nusu fainali au baada ya mchezo kuisha
tegemeana na mtiririko wenu upo vipi.
Kumwelewa
Mwenzi wako.
Tendo la
ndoa lina lugha yake… Tendo hili haliishi tu katika kufurahia na kufika
kileleni bali pia linasaidia kumwelewa na kumsoma mwenzi wako.
Ndio maana ni
vema sana kumjulia mwenza wako kitabia na mwenendo kwa kuhusisha tendo hilo.
Ikiwa wenza mna tabia ya kushirikiana na kuhusishana katika masuala ya kila
siku ni rahisi kutambua kuwa mwenza wako siku hiyo kachoka, kachukizwa (iwe na
wewe ama mtu mwingine), ana mawazo, ana wasiwasi, hana raha n.k.
Haijalishi
kuwa mwenza wako yupo katika hali ipi wengi hujitahidi hilo lisiwe kikwazo kwa
tendo la ndoa (hasa wanaume) – Hivyo ni rahisi kumjulia tokana na namna
mnavyokuwa faragha kujua kuna jambo ama la.
Ni wazi wakati mwingine kunaweza
kuwa na jambo na mwenzi wako asikuhusishe, kupitia tendo la ndoa unaweza pata
viashiria.
Inasaidia
wanandoa kupata Watoto.
Watoto wana
raha yake katika ndoa, na wana nafasi kubwa sana katika kuweza kuimarisha ndoa,
kuleta furaha katika familia, kuwajenga na kuwa komaza kama wazazi na pia
kuwaunganisha zaidi wanandoa kama mwili mmoja.
Si wote wamejaaliwa kupata
watoto (my heart goes out to them) – ila ukweli ni kuwa mara nyingi hiki ni
kipengele muhimu katika ndoa ambacho wanandoa wenyewe na jamii hutarajia kuwa
muhimu kufanikisha ili ndoa ionekane kuwa ina mafanikio.
Niongeze kuwa
tumepishana kutafsiri mafanikio ni nini katika ndoa, ila wengi huwa na msimamo
wa kuwa watoto ni muhimu katika ndoa.
Kutatua
ugomvi/mgogoro kati ya wenza.
Ugomvi
haukwepeki hata kama mwapendana vipi (ingawa frequency ya ugomvi
hupishana kati ya wanandoa). Tendo la ndoa linazungumza mambo mengi sana….
Kitendo cha kukutana kimwili na mwenza wako kwa namna moja wapo inakuwa ni
akili na mwili wako kukubali kuwa umejitoa kwa mwenzi wako kwa wakati huo.
Kuna
makabila ambayo hata uwe umegombana vipi na mke/mume wako, ikitokea tu ukalala
naye na kufanya tendo la ndoa haijalishi kosa lilikuwa ni lipi inachukuliwa
limesamehewa na yapaswa kusahau na kusonga mbele.
Kupunguza
uchovu/Msongo wa mawazo.
Ndoa ni moja
ya njia kwa baadhi kuweza kupunguza uchovu alio nao na kwa wengine hata msongo
wa mawazo.
Tendo likifanywa vema na kwa ustadi, huweza kumwondolea mwenzi wako
uchovu au msongo wa mawazo kwa kiwango kikubwa.
Unafuu huo utegemea lakini,
wengine inakuwa tu unafuu wakati wa tendo hilo na hali wengine hupata nafuu ya
muda mrefu.
Hivyo ikiwa mwenzi wako yupo katika hali hiyo katika kutafuta
namna ya kuhakikisha anapata unafuu, unaweza tumia tendo la ndoa kama silaha ya
kumrudisha mwenzi wako katika hali nzuri.
Linajenga
heshima ndani ya ndoa (hasa kwa wanaume).
Hili
linawezekana pande zote (mke na mume) mmelipa umuhimu wa pekee tendo la ndoa
hadi mkiwa faragha wote hufurahia tendo hili hadi kuna wakati mwajihisi mpo
mwili mmoja kama si ndani ya ngozi moja.
Tunarudi palepale, kuwa ni muhimu
ukampenda mtu wako, ukapenda hilo tendo, mengine yanafuata mkiwa faraghani.
Linatumika
kupata unachotaka/Kulaghai (hasa kwa wanawake).
Hili
linategemea unalifanya kwa namna ipi… Ukilifanya kana kwamba ni hongo ya lazima
na kuwa wamaanisha hutokubali kuwa faragha bila kutimiziwa kitu Fulani – Hapo
inakuwa ni tatizo na ndio ulaghai wenyewe.
Ila lifanywapo kwa upendo, utani wa
kimapenzi, kwa kutoa maneno matamu na kubembembeleza, husaidia kuongeza ashiki
kwa wapenzi (inaweza isiwe kwa wote) na huku pia ukifanikiwa kupata kile
ambacho unataka mwenzio akiwa katika mood nzuri.
Wapendwa
nakaribisha mawazo, michango, maswali, na maoni toka kwenu.
Source Na:- Asha D. Abinallah
No comments:
Post a Comment