Akiongea na
Globu ya Jamii hii iliyofika katika eneo hilo, meneja wa Bandari ya Kilwa, Bw.
Iddi Omary, alieleza kuwa Meli hiyo iliyofunga gati jana jioni ikitokea
songosongo na kupakia tani 30 za mchanga na tani 30 za maji ilizama majira ya
saa 6 usiku wa kuamkia (Desemba 08,2013) ambapo Nahodha wa Meli hiyo Captain Charles
Kalinga na wasaidizi wake 3 walifanikiwa kutoka ila Nice Mtega aliekuwepo ndani
hajaonekana hadi sasa. Juhudi za kumtafuta na kuinua meli hiyo zinaendelea.
Sababu ya kuzama kwake bado hazijajulikana.
Taarifa zaidi => http://bit.ly/1jzyS4J
No comments:
Post a Comment