Tanzania yapanda nafasi moja hadi nafasi ya 127 katika Listi ya Ubora Duniani . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, September 12, 2013

Tanzania yapanda nafasi moja hadi nafasi ya 127 katika Listi ya Ubora Duniani .



Shirikisho la Soka Duniani FIFA leo (Septemba 12,2013) Limetoa Listi ya Ubora Duniani na Mabingwa wa Dunia, Hispania, bado wako pale pale wakishika Nambari Wani huku Tanzania ikipanda Nafasi moja na kushika Nafasi ya 127 lakini kwenye 10 Bora kuna mabadiliko makubwa.


Argentina imeibwagaUjerumani na kuikamata Nafasi ya Pili, Uruguay imepanda Nafasi 5 na sasa ipo ya 7 huku Portugal ikiporomoka kutoka Nafasi 4 na kutua Nafasi ya 11.

Katika 10 Bora zipo Nchi za Marekani ya Kusini 4.

Kwa Nchi za Afrika, Nchi ambayo iko Nafasi ya juu kabisa ni Ivory Coast ambayo iko Nafasi ya 19 ikiwa imeporomoka Nafasi moja na kufuatiwa na Ghana iliyobaki Nafasi ya 24 kama Mwezi uliopita.

Listi ya Ubora inayofuata itatolewa hapo Oktoba 17.


LISTI YA UBORA YA FIFA:-20 BORA.

1        Spain
2        Argentina
3        Germany
4        Italy
5        Colombia
6        Belgium
7        Uruguay
8        Brazil
9        Netherlands
10      Croatia
11      Portugal
12      Greece
13      Marekani -USA
14      Switzerland
15      Russia
16      Chile
17      England
18      Bosnia-Herzegovina
19      Côte d'Ivoire
20      Ecuador

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad