![]() |
Steven
Gerrard (kulia) na Joe Allen
wakishangilia
baada ya bao la kwanza.
|
Liverpool imeshinda 2-0 dhidi ya Olympiakos ya Ugiriki
katika mchezo maalum wa kumuaga Nahodha wake, Steven Gerrard baada ya
kuitumikia klabu kwa miaka 15.
Mabao ya
Wekundu hao wa Anfield katika mchezo huo yalifungwa na Joe Allen dakika ya 23
na Henderson dakika ya 62.
Kikosi cha
Liverpool kilikuwa: Mignolet/Jones dk85 Johnson, Toure/Carragher dk62, Agger,
Enrique; Allen/Henderson dk62, Gerrard/Spearing dk85, Lucas, Coutinho/Fowler
dk72, Sterling/Alberto dk72 na Aspas/Suarez dk62.
Olympiacos:
Megyeri, Maniatis, Fejsa, Mitroglou/Saviola dk56, Samaris/Weiss dk46, Holebas,
Medjani/Manolas dk56, Slovas, Siovas, Campbell, Salino na Dominguez.
![]() |
Jordan
Henderson alifunga la pili kwa Liverpool,ikiwa tu ni sekunde 12 baada ya
kuingia uwanjani.
|
![]() |
Luis Suarez alicheza kwa Liverpool jana(Agosti 03,2013). |
Nao
wachezaji Wayne Rooney, Nani, Nemanja
Vidic na Javier Hernandez wote walianza kikosini Manchester United katika
mchezo wa kirafiki dhidi ya Real Betis ambao mashabiki hawakuingia Uwanja wa
Carrington.
![]() |
Rooney alicheza dhidi ya Real Betis. |
Mshambuliaji
wa England, Rooney alicheza kipindi cha kwanza lakini hakuweza kufunga bao,
mabingwa hao wa Ligi Kuu England wakishinda 3-0.
Mchezo huo
uliochezwa asubuhi ya jana(Agosti 03,2013) kwenye Uwanja huo wa mazoezi wa
United, ulikuwa wa kwanza kwa Rooney baada ya kuumia katika mechi ya kwanza ya
ziara ya Mashariki ya Mbali mwezi uliopita.
Mshambuliaji
huyo mwenye umri wa miaka 27, ambaye hajatulia, amepona maumivu ya nyama za
paja aliyoyapata katika ziara ya Asia ya klabu hiyo na jana alionyesha yuko
sawa akicheza dhidi ya timu hiyo ya La Liga.
Rooney
anatarajiwa kuhama Old Trafford kutimkia Chelsea, ambao ofa yao ya pili ya
Pauni Milioni 23 ilipigwa chini.
Anaweza kuwa
na mazungumzo zaidi na kocha David Moyes wiki ijayo juu ya mustakabali wake
wakati United ikijiandaa kwa mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya AIK mjini
Stockholm.
Lakini
United inabaki na msimamo wake wa kumbakiza.
![]() |
Beki Nemanja Vidic akipambana na George Ray wa Crewe Jumatatu. |
![]() |
Vidic alianza jana (Agosti 03,2013) katika mchezo ambao ulichezwa milango imefungwa. |
No comments:
Post a Comment