Arsenal FC wamenusurika na kupata Sare ya Bao 2-2 na Napoli katika Mashindano ya kugombea Emirates Cup. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, August 04, 2013

Arsenal FC wamenusurika na kupata Sare ya Bao 2-2 na Napoli katika Mashindano ya kugombea Emirates Cup.

Giroud aliifungia Arsenal  bao la Kwanza kwa tik tak  Dakika ya 71  kabla ya mechi yao iliyoisha kwa  Arsenal kutoka 2-2 na Napoli katika Mashindano ya kugombea Emirates Cup yanayochezwa Uwanjani kwao Emirates Jijini London.


Gonzalo Higuain akikabiliana na Laurent Koscielny

Pandev akishangilia bao la pili aliloifungia Napoli  Dakika ya 29 kabla ya mechi yao iliyoisha kwa  Arsenal kutoka 2-2 na Napoli katika Mashindano ya kugombea Emirates Cup yanayochezwa Uwanjani kwao Emirates Jijini London.

Lorenzo Insigne akishangilia bao la kwanza aliloifungia Napoli  Dakika ya 7 na Pandev Dakika ya 29 kabla ya mechi yao iliyoisha kwa  Arsenal kutoka 2-2 na Napoli katika Mashindano ya kugombea Emirates Cup yanayochezwa Uwanjani kwao Emirates Jijini London.

Wachezaji wakiwa wamemzingira refa baada ya Arsenal kupewa penalti, ambayo iliokolewa na Pepe Reina (wa pili kushoto) baada ya Lukas Podolski kupiga.

Arsene Wenger (kulia) akisalimiana na Rafael Benitez (kushoto) kabla ya mechi yao iliyoisha kwa  Arsenal kutoka 2-2 na Napoli katika Mashindano ya kugombea Emirates Cup .
KLABU ya Arsenal jana ilitoka nyuma kwa mabao mawili na kupata sare ya 2-2 mbele ya timu ya kocha Rafael Benitez, Napoli katika mchezo wao wa kwanza wa Kombe lao la Emirates.

Lorenzo Insigne na Goran Pandev waliwafungia mabao wageni kipindi cha kwanza, katika mchezo huo wa kujiandaa na msimu, Gunners wakionekana kuzidiwa kipindi cha kwanza.

Hata hivyo, The Gunners walizinduka na kufanikiwa kusawazisha mabao yote, moja la Olivier Giroud kwa tika tak dakika ya 71 na lingine Laurent Koscielny kwa kichwa dakika ya 85, baada ya Insigne kufunga dakika ya saba na Pandev dakika ya 29.


Arsenal walipata nafasi ya kufunga bao la tatu, lakini mkwaju wa penalti wa Lukas Podolski uliokolewa na kipa Pepe Reina wa Napoli.



EMERATES CUP 2013.
RATIBA:

[Saa za Bongo] 

Jumamosi Agosti 3

Galatasaray Spor Kulübü – Turkey 0 FC Porto – Portugal 1

Arsenal FC – England 2 Napoli – Italy 2  

Jumapili Agosti 4

15:00 Napoli – Italy v FC Porto - Portugal

17:20 Arsenal FC – England v Galatasaray Spor Kulübü - Turkey


Katika Mechi iliyochezwa mapema, FC Porto ilifungwa Bao 1-0 na Galatasaray kwa Bao la Mbrazil Felipe Melo la Dakika ya 71.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad