Tazama Picha za Makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru 2013 kati ya Mkoa wa kagera na Kigoma (Julai 09,2013) kwenye Mpaka wa Wilaya ya Biharamulo na Kakonko. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, July 13, 2013

Tazama Picha za Makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru 2013 kati ya Mkoa wa kagera na Kigoma (Julai 09,2013) kwenye Mpaka wa Wilaya ya Biharamulo na Kakonko.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Masawe  na  mwenzie Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Luteni Kanali mstaafu Issa Machibya  wakikabidhiana  Mwenge wa Uhuru  uliohitimisha mbio zake  Mkoani  Kagera  (Julai 09,2013)  katika wilaya ya Biharamulo na kukabidhiwa Mkoani Kigoma kupitia wilaya ya Kakonko.



Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Masawe  na  mwenzie Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Luteni Kanali mstaafu Issa Machibya  wakikabidhiana  Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma.



Mwenge.......chomaaa......chomaaaa........ Makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru 2013 kati ya Mkoa wa kagera na Kigoma (Julai 09,2013)  kwenye Mpaka wa Wilaya ya Biharamulo na Kakonko.





 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Luteni Kanali mstaafu Issa Machibya wa  kwanza mbele,Huku Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Bw.Petter Toima wakisubiri kukabidhiwa  Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ili kuanza mbio zake Mkoani Kigoma(Julai 09,2013 hadi Julai 16,2013).

Baadhi ya Wananchi waliojitokeza kushuhudia Makakabidhiano ya  Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ili kuanza mbio zake Mkoani Kigoma(Julai 09,2013 hadi Julai 16,2013).

Baadhi ya Viongozi wa Serikali na Chama wa Mkoa wa Kigoma wakisubiri kukabidhiwa  Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ili kuanza mbio zake Mkoani Kigoma(Julai 09,2013 hadi Julai 16,2013).

Wanajeshi nao wa jeshi la Kujenga Taifa (JKT-Kanembwa wilayani Kibondo mkoani Kigoma) nao walijitokeza kuonyesha uzalendo wao wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ili kuanza mbio zake Mkoani Kigoma(Julai 09,2013 hadi Julai 16,2013).

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali Issa Machibya akiwa anasikiliza kwa makini hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Fabiani Massawe wakati wa makabidhiano ya   Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ili kuanza mbio zake Mkoani Kigoma(Julai 09,2013 hadi Julai 16,2013).


Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Masawe akisoma Hotuba wakati wa makabidhiano ya  Mwenge wa uhuru (Julai 09,2013)  kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali Mstaafu Issa Machibya, na kusema kuwa  Mwenge huo ukiwa Mkoani Kagera umepitia miradi 78  ya Maendeleo ya Wananchi iliyogharimu jumla ya Shilingi Bilioni 11.5 .



Mdau wa Blog ya Mwana wa Makonda na Mwandishi Shabani Ndyamukama katikati akiwa na wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2013,kulia Bw.Seperatus Lubinga na Bi.Zamda John katika picha ya pamoja katika shule ya sekondari Kinyonza wilayani Kakonko mkoani Kigoma.

Juu na Chini ni Baadhi ya Vikundi vya Ngoma za Asili vikitumbuiza wakati wa makabidhiano ya   Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ili kuanza mbio zake Mkoani Kigoma(Julai 09,2013 hadi Julai 16,2013).


Baadhi ya Viongozi wa wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera wakiwa katika harakati mbalimbali wakati wa makabidhiano ya   Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ili kuanza mbio zake Mkoani Kigoma(Julai 09,2013 hadi Julai 16,2013).


Mkuu wa wilaya ya Ngara Mkoani Kagera Bw.Kostantine Kanyassu(Mwenye miwani)akiagana na wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka huu 2013 wakati wa makabidhiano ya   Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ili kuanza mbio zake Mkoani Kigoma(Julai 09,2013 hadi Julai 16,2013).

Msafara wa magari ukiwa umepati pembeni wakati wa makabidhiano ya   Mwenge wa Uhuru  katika  Mpaka  wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera na  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma ili kuanza mbio zake Mkoani Kigoma(Julai 09,2013 hadi Julai 16,2013)Picha na Shabani Ndyamukama.


Mbio za Mwenge wa Uhuru zilizoanza Mkoani  Kagera  (Julai 01,2013) zimehitimishwa (Julai 09,2013)  katika wilaya ya Biharamulo na kukabidhiwa Mkoani Kigoma kupitia wilaya ya Kakonko .




Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Masawe akikabidhi Mwenge huo (Julai 09,2013)  kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali Mstaafu Issa Machibya, amesema Mwenge huo ukiwa Mkoani Kagera umepitia miradi 78  ya Maendeleo ya Wananchi iliyogharimu jumla ya Shilingi Bilioni 11.5 ,ikiwa ni Fedha zitokanazo na Nguvu za Wananchi,Serikali  Kuu,Halmashauri  na  Wahisani.




Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Luteni Kanali mstaafu Issa Machibya  alisema Jumla ya miradi 64 yenye thamani ya Shilingi  Bilioni  13.7 itapitiwa na Mbio  hizo za Mwenge  wa Uhuru kwa Mwaka huu 2013 kwa kukimbizwa Wilaya Saba za Mkoa huo ambapo ukihitimisha mbio zake(Julai 16,2013)  utakabidhiwa Mkoani  Katavi. 




Akiwaaga Viongozi wa Mkoa wa Kagera na kuingia Mkoani Kigoma ,Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa mwaka huu 2013, Bw Juma Ally Sumai alisema kuwa amefurahishwa na mshikamano pamoja na Ushirikiano uliopo kwa viongozi  na watendaji mkoani Kagera  katika kusimamia na kuleta maendeleo kwa wananchi.



Dr. Ali Mohamed Shein.
Aidha Mwenge wa uhuru uliwashwa (May 06,2013) mjini Pemba katika Kijiji cha Chokocho na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein na unatarajiwa kuhitimisha mbio zake Mkoani  Iringa october 14,2013.


Kauli mbiu ya Mwaka huu 2013 katika Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru ni''Watanzania ni wamoja''Tusigawanywe kwa Misingi ya tofauti zetu za Dini,Itikadi,rangi na Rasilimali''


This year’s race also coincide with the ”50th anniversary of Zanzibar’s Revolution.Other message to be promoted during the race included;” Fight against HIV/AIDS and drugs use” and “Fight against corruption” The Uhuru Torch is one of  Tanzania’s national symbols.It  symbolizes freedom and hope.
 




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad