Taarifa mpya zinakanusha habari za Saida kalori, Zinasema hakufariki dunia na Kweli ajali ya boti imetokea lakini Saida hakuwemo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, June 19, 2013

Taarifa mpya zinakanusha habari za Saida kalori, Zinasema hakufariki dunia na Kweli ajali ya boti imetokea lakini Saida hakuwemo.



Saida Karoli.
Taarifa ya Neville Meena imesema kuwa ingawa ni kweli kuna ajali ya boti iliyotokea, mwanamuziki Saida karoli hakuwa mmoja wa waliokuwemo kwenye boti hiyo na yuko hai.




Taarifa hiyo imetoa angalizo kutafuta uhakika kwani inasemekana kuwa Saida Karoli ni mzima, yupo jijini Dar es Salaam: “Nimetafuta namba yake ya simu sijaipata, ila taarifa kutoka Bukoba na ofisi ya Ofisa Utamaduni Muleba zinasema siyo kweli…” ameandika Meena.




Kuhusiana na ajali ya boti, Meena amesema, “…ni kweli kwamba kuna boti imezama katika Ziwa Victoria, na kulikuwa na uvumi mwingi mjini Bukoba na Wilayani Muleba kuhusu mwanamuziki huyo kufariki lakini baadaye ikathibitika kwamba hakuwa mmoja wa abiria.”


Aidha katika taarifa za awali zilisema kwamba’’,…Mwanamuziki Saida Karoli amefariki  baada ya kuzama kwenye maji kufuatia  boti aliyokuwa akisafiri nayo toka Kisiwa cha Goziba kuzama baada ya  kukumbwa na dhoruba na kuzama Ziwa Victoria.

Inaalifiwa pamoja naye kuna watu wengine wamefariki dunia.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad