Waganga
na wakunga wa tiba asilia katika Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, wametakiwa
kuzingatia usafi wa vifaa wanavyovitumia katika kutoa tiba kwa wananchi, ili
kuepuka kueneza magonjwa kutokana na uchafu wa vifaa hivyo.
Mkuu
wa wilaya ya Bukoba mkoani Kagera Bw.Zipporah Pangani ametoa wito huo wakati wa mkutano wa kukabidhi
vyeti vya Serikali kwa waganga 13, ambavyo vinawaruhusu kufanya kazi ya kutoa
tiba kwa jamii kisheria,katika katika Uwanja wa Uhuru mjini Bukoba.
Amesema
waganga hao wasipozingatia usafi wa vifaa vyao wanaweza kusababisha kuenea kwa magonjwa kama
Ukimwi na kuharisha.
Bw.
Pangani amewataka waganga kuongeza ujuzi na kuboresha shughuli zao kwa kutumia
dawa hizo kutengeneza vidonge na kuitaka jamii kutambua kazi zinazofanywa na
waganga hao, maana zipo kwa mujibu wa sheria namba 23 ya mwaka 2002.
Naye
Mwenyekiti wa Chama cha Waganga na
Wakunga wa Tiba Asilia (STAMATA) Manispaa ya Bukoba,Bw. Habibu Mahyoro amesema watu wanaoishi kwa kutegemea viungo
vya binadamu si waganga bali ni matapeli
na ni wachawi.
Ameiomba
Serikali kuwawezesha kupata vitendea kazi, ikiwamo vyombo vya usafiri ambavyo
vitatumika kutoa elimu kwa jamii kwa lengo la kupunguza matukio ya
wanaojihusisha na matendo maovu ikiwamo mauaji ya albino na vikongwe.
Awali
akisoma risala kwa mgeni rasmi Katibu wa kamati ya maandalizi, Bi.Veidiana
Lukeisa amesema waganga wana umuhimu
mkubwa, kwani yapo baadhi ya magonjwa ndani ya jamii ambayo hutibiwa na dawa za
asili pekee.
Ameiomba
Serikali kuwashirikisha ili kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwamo kupambana na magonjwa kama malaria na
Ukimwi kwa kutumia tiba asilia na kutoa
ushauri.
Pia
ameiomba Serikali kuweka utaratibu utakaosaidia hospitali kuwapokea wagonjwa
kutoka kwa waganga na wakunga wa tiba asilia, ili kupunguza vifo vinavyoweza
kuzuilika.
Aidha
STAMATA mkoani Kagera ilianzishwa mwaka 2011 ikiwa na wanachama 47 ambapo mpaka sasa ina wanachama 89 kutoka wilaya za
Misenyi na Bukoba.






No comments:
Post a Comment