Tabia ya utoro bungeni imejirudia tena mwaka huu wakati Bunge likijadili Bajeti ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, April 24, 2013

Tabia ya utoro bungeni imejirudia tena mwaka huu wakati Bunge likijadili Bajeti ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.



Bungeni Dodoma.
Tabia ya utoro bungeni imejirudia tena mwaka huu wakati Bunge likijadili Bajeti ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika. 
 


Safari hii utoro huo unawahusisha mawaziri na siyo wabunge.




Tukio kama hilo liliwahi kutokea Julai 22, mwaka jana wakati wa mjadala wa Bajeti wa Wizara hiyo kiasi cha kufanya moja ya vikao vyake kuahirishwa kutokana na utoro wa wabunge.




Kufuatia utoro huo, Mbunge wa Mwibala CCM KANGI LUGORA ameomba muongozo wa Spika juu ya kitendo hicho anachodai kuwanyima haki wananchi.



Akiomba mwongozo huo LUGORA amesema, licha ya Wizara hiyo kuwa na masuala yanayomgusa moja kwa moja mwananchi wa chini ambaye ni mkulima, mahudhurio ya mawaziri hayaridhishi huku akikiomba kiti kuhairisha kujadiliwa kwa bajeti hiyo.






Job Ndugai.
Akitolea ufafanuzi muongozo huo Naibu Spika wa Bunge JOB NDUGAI anabainisha kuwa, Mawaziri wote wapo mjini Dodoma wakijiandaa tayari kwa uwasilishaji wa bajeti za Wizara zao.
 

Hata hivyo baadhi ya Wabunge wakichangia bajeti hiyo akiwemo SELEMANI BUNGARA na JOHN CHEYO wameitaka Serikali kuurekebisha mfumo wa Stakabadhi ghalani kwani badala ya kuwa mkombozi umeendelea kuwadidimiza wakulima kiuchumi.




Utoro Bungeni.
Julai 22 mwaka jana, Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia alisimama kuomba mwongozo wa Naibu Spika, Job Ndugai kutokana na Bunge kutokuwa na nusu ya wabunge wote kinyume cha Kanuni ya Bunge wakati wa Bajeti ya Wizara hiyo ya Kilimo, Chakula na Ushirika.



Idadi ya wabunge wote ni 352 lakini wabunge waliomo humu ndani haizidi 110, ambapo nusu ya wabunge wote ni 176 hivyo kuendelea kupitisha bajeti hiyo ni kuvunja kanuni,” alisema Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi.



Baada ya kujiridhisha kwamba idadi hiyo ilikuwa ndogo, Naibu Spika aliahirisha kupitishwa kwa Bajeti hiyo.



 Bajeti hiyo ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika imehitimishwa leo tayari kwa Bajeti ya Wizara ya Maji kuanza kujadiliwa hapo kesho.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad