![]() |
| Kigoma |
Naibu Waziri
wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima, alibainisha hayo bungeni jana(April
22,2013) alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kasulu Vijijini, Agripina
Buyogera, aliyetaka kujua ni lini serikali itajenga soko la uhakika kwa ajili
ya wakulima wa Kasulu.
Waziri Malima
alisema hatua iliyofikiwa na serikali katika kujenga soko hilo ni halmashauri
kusaini Mkataba wa Maelewano (MoU) na Benki ya Rasilimali (TIB) Mei mwaka 2012
ambayo imekubali kuchangia asilimia 80 ya gharama za ujenzi huku Kasulu
itachangia asilimia 20.
Kwa mujibu
wa naibu waziri huyo, soko kuu la mazao wilayani humo linatarajiwa kujengwa
kwenye eneo lililopo katikati ya vijiji vya Mgombe na Nyachenda.
Kuhusu
kuondoa migogoro ya ardhi hususan katika eneo litakalojengwa soko hilo,
serikali wilayani Kasulu imekamilisha uwekezaji wa maeneo hayo kwenye mpango wa
matumizi bora ya ardhi katika vijiji hivyo kabla ya ujenzi huo kuanza.
Pia Malima
alitolea ufafanuzi kuhusu tuhuma za baadhi ya watendaji kutokuwa waaminifu
katika ukusanyaji wa ushuru ambapo alisema wizara kwa kushirikiana na idara na
taasisi, itafanya jitihada zote kupambana nao.
Alikiri kuwa
watendaji hao wamekuwa wakiwatoza ushuru wakulima mara mbili kutokana na sababu
mbalimbali ikiwamo kuuza mazao yao bila ya kudai au kupewa stakabadhi za malipo
au kulipa ushuru sehemu ndogo ya mazao hivyo kulipishwa mara mbili.
“Mheshimiwa
Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu inatoza ushuru kwa kuzingatia Sheria ya
Fedha za Serikali za Mitaa Na. 9, kifungu cha 7(1) (g) ya mwaka 1982 ambayo
ushuru unaotozwa ni kati ya asilimia 3 na 5 ya bei ya shambani,” alisema.
Chanzo:Tanzania
Daima.






No comments:
Post a Comment