Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imetinga rasmi bungeni asubuhi hii April 11, 2013. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, April 11, 2013

Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imetinga rasmi bungeni asubuhi hii April 11, 2013.



Ile ripoti maarufu kuliko zote, ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (RIPOTI YA CAG), imetinga rasmi bungeni asubuhi hii, na kwa mujibu wa sheria mpya ya CAG iliyopitishwa mwaka jana, ilibidi na serikali kuwasilisha majibu ya hoja za CAG sambamba na taarifa hiyo ya CAG, kitu ambacho serikali haikufanya.


Mbunge wa Bariadi, Mhe. John Memosa Cheyo, amesimama kuomba muongozo wa spika, serikali inapovunja sheria siku ya kwanza ambayo ilitakiwa ianze kutekelezwa!. Spika akaomba majibu kwa waziri na mwanasheria mkuu, wote hawakuwa na majibu!, amewapa mpaka mchana serikali ilete majibu!.


Kwa msiokumbuka, ni RIPOTI YA CAG ya mwaka jana, ilileta songombwingo na patashika ya mashati kuchanika kule bungeni Dodoma kwa serikali kuponea chupu chupu kuvunjwa kwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Spika akaikingia kifua, na JK akakubali matokeo kwa kulivunjilia mbali baraza la mawaziri, na kuwatosa mawaziri wenye makandokando yaliyoichafua serikali ya JK, hivyo kuunda baraza jipya ambalo sasa ni la serikali safi!, na kama itaendelea kwa usafi huu, kutakuwa na haja kweli ya kuibadili seririkali mwaka 2015?.




Kwa wafuatiliaji makini, ripoti hizi zinapatikana online kwenye website ya NAOT   National Audit Office of Tanzania
 
Financial Year 2011/2012 11 Apr 2013



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad