Kocha Jose Mourinho ameitaka Chelsea kuthibitisha kurejea kwake Stamford Bridge licha ya kuwindwa na klabu za Manchester City, Paris Saint-Germain na AC Milan . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, April 07, 2013

Kocha Jose Mourinho ameitaka Chelsea kuthibitisha kurejea kwake Stamford Bridge licha ya kuwindwa na klabu za Manchester City, Paris Saint-Germain na AC Milan .



Jose Mourinho
Kocha Jose Mourinho ameitaka Chelsea kuthibitisha kurejea kwake Stamford Bridge au kujiweka hatarini kumkosa.



Kocha huyo wa Real Madrid anatarajiwa kumpokea majukumu Rafa Benitez mwishoni mwa msimu hiyo ikiwa mara ya pili kwake kufanya kazi Ligi Kuu England.


Lakini Manchester City, Paris Saint-Germain na AC Milan pia zimeripotiwa kumsubiri mkali huyo wa mataji.





Muda unakimbia: Jose Mourinho amejiandaa kurejea Chelsea mwishoni mwa msimu.



"Jose anataka kurudi Chelsea. Ni mahali anapotaka kuwa," chanzo kimeiambia The Sun.


"Kila wakati mashabiki wa Chelsea wanaimba jina lake na hiyo inamfanya atake kurejea hata zaidi.


"Atasaini kwa dau lile analopata Real, pamoja na kwamba ana uhakika wa kupata zaidi sehemu nyinginekama City au PSG.


Real Madrid wakianza bila Nyota wao Ronaldo, Real walijikuta wakitanguliwa Bao 1-0 na Levante katika Mechi iliyochezwa Uwanjani Santiago Bernabeu lakini walizinduka na kufunga Bao mbili za haraka kupitia Gonzalo Higuain na Penati ya Kaka.




Ronaldo aliingizwa Kipindi cha Pili na kupiga Bao moja na nyingine mbili kuongezwa na Mezut Ozil.




Jumanne ijayo  Real Madrid watakuwa huko Uturuki kurudiana na Galatasaray katika Robo Fainali ya UEFA huku wao wakiwa washindi wa Bao 3-0 katika Mechi ya kwanza.





"Jose anaweza pia kubaki Madrid, lakini yuko wazi juu ya wapi anapotaka kwenda — sasa ipo juu ya Roman Abramovich ikiwa anataka hivyo.'



Mourinho ameshinda mataji sita na Chelsea ndani ya misimu mitatu, lakini hakuweza kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa.



Anatarajia kufanya hivyo Uwanja wa Wembley, Mei 25 akiwa na Real Madrid ambayo ina matumaini ya kuingia Nusu Fainali baada ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Galatasaray wiki iliyopita.



Rafa Benitez
Safari inanukia: Rafa Benitez anatarajiwa kuachia ngazi mwishoni mwa msimu.



Benitez hajawahi kukubalika kwa imani za Chelsea, baada ya kuchukua mikoba ya Roberto Di Matteo, aliyetupiwa virago.



Mspanyola huyo ameweka bayana ataachia ngazi mwishoni mwa msimu, lakini atakuwa bado hajatwaa mataji ya Europa League na Kombe la FA.
 

 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad