Kampuni ya usafirishaji
ya Sultani Salim ya jijini Dar es Salaam,imeanza ujenzi wa nyumba ya Bi.Bibiana John mkazi wa Kumuyange wilayani Ngara
mkoani Kagera, ambayo iligongwa na
kubomolewa na gari la kampuni hiyo katika ajali iliyotokea siku ya Jumamosi(April
13,2013) jumaa lililopita.
Wakala wa
Kampuni hiyo Bw.Martin Raphael ameiambia Redio Kwizera FM kuwa tayari
maandalizi ya ujenzi wa nyumba mpya kwa ajili ya Mhanga huyo na familia yake
umeanza.
Bw. Rafael
amesema kuwa pamoja na shughuli ya ujenzi wa nyumba hiyo, kampuni hiyo pia imeshiriki
kufanya mazishi ya watu wawili waliopoteza maisha katika ajali hiyo.
Amesema kuwa
kampuni hiyo imetoa rambi rambi ya shilingi laki moja kwa kila familia na kuongeza
kuwa kampuni hiyo itatoa fidia ya piki piki iliyogongwa katika ajali hiyo baada ya kupata taarifa ya mkaguzi wa polisi kitengo cha usalama barabarani.
 |
Aidha watu
wawili walifariki dunia papo hapo na
wengine wawili kujeruhiwa baada ya gari hilo aina ya Mercedec benz lenye namba ya
usajili T 908 ABZ semitrailer lililokuwa ikitokea nchini Burundi, kuacha njia (April
13,2013) muda wa saa 12 jioni na kupinduka katika eneo la Kumuyange nje kidogo
ya mji wa Ngara mkoani Kagera.
Kwa mujibu
wa Kamanda wa Polisi wilaya ya Ngara
Abel Mtagwa aliwataja watu hao waliofarki katika ajali hiyo kuwa ni
Edward Filimon alie kuwa akiendesha pikipiki yake yenye namba za usajiri T 756
BZJ na abiria wake ambae hadi sasa haja fahamika jina lake.
|

 |
Kamanda
Mtagwa aliwataja majeruhi wa ajari hiyo kuwa ni Dereva wa gari hilo Hajji Omary
Ibrahim(29) mkazi wa gongolamboto jijini Dar es salaam ambaye amaruhusiwa baada ya kutibiwa na tingo
wake aliyejulikana kwa jina la Kambi simba(40) ambaye bado anaendelea kupata
matibabu katika Hospital ya Murugwanza wilayani Ngara mkoani Kagera.
Aidha chanzo
cha ajari hiyo ni gari hilo kufeli mfumo wa Breki jambo ambalo Dereva wake alishindwa kulimudu
kuliendesha ndipo lilipanda mtaro na kubomoa nyumba hiyo.
|
No comments:
Post a Comment