Makadinali wa Kanisa katoliki |
Asubuhi ya leo (March 12,2013) Makadinali 115
watashiriki katika misa ya pamoja kabla ya kuanza mchakato wa kumtafuta
kiongozi mpya kuanzia jumanne hii.
Makadinali
hao watapiga kura mara nne kila siku hadi theluthi mbili watakapo kubaliana
kuhusu ni nani atakayekuwa kiongozi wao.
Papa
Emeritus aliyekuwa
akifahamika
kama Papa
Benedicto
wa 16 kabla
ya
kujiuzulu nafasi yake.
|
Wakati wote
wa uchaguzi huo Makadinali hao watajifungia katika chumba maalum hadi pale
makadinali 77 watakapoafikiana kuhusu Papa mpya.
Zoezi hili
huenda likachukua siku kadhaa na papa atakayechaguliwa atakuwa papa wa 266 wa
kanisa hilo na kuwaongoza wakatoliki takribani bilioni 1 nukta mbiili duniani
kote.
Papa Mpya
atachukua nafasi ya Papa Emeritus zamani akifahamika kama Benedicto wa kumi na
sita aliyejiuzulu mwezi uliopita kwa sababu ya umri mkubwa wa miaka 85 na
sababu za kiafya.
No comments:
Post a Comment