Mchakato wa kumpata Papa mpya wa kanisa katoliki waanza mjini Roma . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, March 12, 2013

Mchakato wa kumpata Papa mpya wa kanisa katoliki waanza mjini Roma .

Makadinali  wa Kanisa katoliki
Makadinali  wa Kanisa katoliki Duniani wamekutana mjini Roma nchini Italia kuanza zoezi la kumchagua Papa mpya wa kanisa hilo atakayeziba pengo lililoachwa na Papa Benedicto wa kumi na sita aliyejiuzulu rasmi mwishoni mwa mwezi uliopita.

 

Asubuhi ya leo (March 12,2013) Makadinali 115 watashiriki katika misa ya pamoja kabla ya kuanza mchakato wa kumtafuta kiongozi mpya kuanzia jumanne hii.



Makadinali hao watapiga kura mara nne kila siku hadi theluthi mbili watakapo kubaliana kuhusu ni nani atakayekuwa kiongozi wao.





Papa Emeritus aliyekuwa

akifahamika kama Papa

Benedicto wa 16 kabla

ya kujiuzulu nafasi yake.

Wakati wote wa uchaguzi huo Makadinali hao watajifungia katika chumba maalum hadi pale makadinali 77 watakapoafikiana kuhusu Papa mpya.




Zoezi hili huenda likachukua siku kadhaa na papa atakayechaguliwa atakuwa papa wa 266 wa kanisa hilo na kuwaongoza wakatoliki takribani bilioni 1 nukta mbiili duniani kote.




Papa Mpya atachukua nafasi ya Papa Emeritus zamani akifahamika kama Benedicto wa kumi na sita aliyejiuzulu mwezi uliopita kwa sababu ya umri mkubwa wa miaka 85 na sababu za kiafya.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad