Hii ndio hoteli ya The Windsor Atlantica, inayojulika iliyopo kwenye fukwe za Copacabana itakayotumiwa na Kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza wakati wa michuano ya Kombe la Dunia 2014. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, March 01, 2013

Hii ndio hoteli ya The Windsor Atlantica, inayojulika iliyopo kwenye fukwe za Copacabana itakayotumiwa na Kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza wakati wa michuano ya Kombe la Dunia 2014.


The Windsor Atlantica

Kikosi  cha timu ya taifa ya Uingereza kimepanga kula maisha Rio de Janeiro wakati wa michuano ya Kombe la Dunia 2014, kwa kuweka kambi yake kwenye hoteli ya The Windsor Atlantica, inayojulika iliyopo kwenye fukwe za Copacabana.




Vijana hao wa kocha  Roy Hodgson wataishi kwenye hoteli hiyo ya nyota tano, ambayo iko pembezoni mwa bahari, wakati wa mechi yao ya kirafiki dhidi ya Brazil kwenye uwanja wa Maracana, Juni 2, mwaka huu.



Eneo la Beach: Hoteli ya England (Jengo refu zaid) ikiangalia fukwe za Copacabana

The Windsor Atlantica yatakuwa makazi ya Uingereza, mwanzoni wa Juni.



Ndani ya hoteli hiyo

ambayo Timu ya Taifa ya

Uingereza watafikia

Wamedhamiria kutumia hoteli hiyo  hiyo wakati wa michuano ya Kombe la Dunia, mwaka mmoja baadaye, iwapo kikosi hicho kitafuzu kushiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014.


 
Jengo la hoteli hiyo ya nyota tano ndilo refu zaidi kwenye eneo lilipo, huku likiangalia fukwe za Copacabana .


 
Moja ya maeneo ya kuvuti Kaskazini mwa Havana: Aidha Timu hiyo ya Taifa ya Uingereza  watakula bata kwenye moja ya maeneo mazuri zaidi ya Rio.








Hoteli hiyo ina vyumba 54  huku Uingereza  wakitarajiwa kuishi kwenye ghorofa ya pili na ya tatu ya hoteli hiyo ambapo  wakiwa hapo watakuwa na sehemu yao maalumu ya kula, matibabu na kujiachia.




Lakini watakutana na wananchi wengi pale watakapokatiza kwenye eneo la mapokezi la hoteli hiyo.



Haitafanana na makao makuu yao ya Kombe la Dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini ambaklo walikaa kwenye hoteli ya Royal Bafokeng Sports Campus iliyopo Rustenburg, hoteli ambayo iliwakera baadhi ya wachezaji.



Hoteli hiyo inasehemu ya spa na bafu linye shower saba kwa ajili ya kupunguza uchovu.



Windsor Atlantica pia wanatoa mataulo ya ufukweni, viti na miamvuli.

 


Kwenye michuano ya Euro mwaka jana nchini Poland, Uingereza waliweka makazi yao katikati ya mji wa Krakow.



Lakini hoteli ya Stary ilichaguliwa mahususi kwenye michuano hiyo kwa sababu za kiusalama kwa sababu kulikuwa na walinzi waliohakikisha wachezaji wanapata muda binafsi.



Wakati wakiwa hawana kazi jijini Rio, Uingereza  watakuwa wakipumzika kwenye fukwe kubwa zaidi duniani za Copacabana.



Na kwa jambo lolote ambalo England watakuwa wanataka kukabiliana nalo juu ya masuala ya Kombe la Dunia, Uongozi wa FIFA utakuwa jirani yao kwenye hoteli ya Copacabana Palace.






No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad