Kocha Mkuu
wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametaja wachezaji 22 watakaoingia kambini Januari 6
mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mechi za kirafiki ikiwa ni sehemu
ya maandalizi ya mechi ya mashindano dhidi ya Morocco itakayochezwa Machi mwaka
huu.
Kwa mujibu
wa Kocha Kim, wachezaji hao wanatakiwa kuripoti kambini katika hoteli ya
Tansoma saa 11.30 jioni tayari kwa mazoezi yatakayoanza Januari 7 mwaka huu.
Wachezaji
walioitwa ni makipa Juma Kaseja kutoka Simba ambaye pia ndiye nahodha wa Stars,
Aishi Manula na Mwadini Ally wote kutoka Azam.
Mabeki ni Aggrey Morris (Azam),
Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Kelvin
Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga) na Shomari Kapombe (Simba).
Viungo ni
Salum Abubakar (Azam), Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Khamis Mcha
(Azam), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba) na Shabani Nditi (Mtibwa
Sugar).
Washambuliaji
ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya
Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), na Thomas Ulimwengu wa
TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Mbali ya
Kim, benchi la ufundi la Taifa Stars linaundwa na Sylvester Marsh (Kocha
Msaidizi), Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja), Dk.
Mwanandi Mwankemwa (Daktari wa timu), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na
Alfred Chimela (Mtunza vifaa).
Aidha pia Shirikisho
la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua ofisa wake Leslie Liunda wa Tanzania
kwenda Ethiopia kukagua viwanja na hoteli ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa
utaratibu wa utoaji leseni kwa klabu zitakazoziwezesha kushiriki michuano
inayoandaliwa na Shirikisho hilo.
Ofisa huyo
atawasili nchini Ethiopia kesho (Januari 2 mwaka huu) ambapo anatarajiwa
kukamilisha kazi hiyo Januari 6 mwakani na baadaye kupeleka ripoti yake CAF.
Utekelezaji
wa kazi yake hiyo nchini Ethiopia utahusisha wadau mbalimbali ikiwemo
Shirikisho la Mpira wa Miguu la Ethiopia (EFF), Wizara ya Michezo ya nchi hiyo,
viongozi wa klabu na mameneja wa viwanja husika.
Boniface
Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
No comments:
Post a Comment