Marehemu
Sadick Juma Kilowoko
'Sajuki'
enzi za uhai wake
.
|
Taarifa
ambazo zimeridhiwa na maamuzi ya familia na ndugu wa karibu pia zimetoka kwa
msemaji wa Bongo Movie na wahusika wa maandalizi ya mazishi hayo, wanasema
ndugu wa Sajuki wameridhia marehemu kuzikwa hapa na sio Songea kama wengine
wanavyotangaza.
Kuhusu
kusogeza mpaka ijumaa, msemaji huyo akasema, ni kutokana na kusubiri ndugu wa
marehemu wanaotoka sehemu mbali mbali kuja Dar es salaam kwa ajili ya mazishi
hayo, wengi wakitokea Songea.
Marehemu
Sadick Juma Kilowoko
'Sajuki'
enzi za uhai wake
akiwa na mkewe Wastara Juma.
|
Marehemu
Sajuki amefariki leo alfajiri Marehemu Sajuki alizaliwa mwaka 1986 mkoani
Ruvuma na ameacha mke na mtoto mmoja wa kike.
YAH: SALAAM
ZA RAMBIRAMBI.
Baraza la
Sanaa la Taifa limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba wa msanii wa
tasnia ya filamu nchini Sadick Juma Kilowoko a.k.a Sajuki.
“ Baraza
limestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa ya kifo hiki cha Sajuki
ambaye mchango wake unahitajika sana katika tasnia ya sanaa, pengo aliloliacha
ni kubwa kwani ubunifu wao bado unahitajika katika tasnia hii.”
Baraza linatoa
pole kwa familia ya marehemu na wasanii wote nchini, aidha linawatakia moyo wa
subira katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na mpendwa wetu.
Tunaomba
mwenyezi Mungu aipumzishe mahala pema peponi roho ya marehemu. Baraza liko
pamoja na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo,
tutambue kuwa haya ni mapenzi ya Mungu.
Imetolewa na
Ghonche
materego
Katibu
Mtendaji
Baraza la
Sanaa la Taifa.
Hii ni clip
niliyoichukua Hotel Arusha wakati Marehemu Sajuki akiwa amepumzishwa baada
yakudondoka stejini na kesho yake akapelekwa Dar kuendelea na matibabu. Hapo
chumbani kulikuwa wasanii wa watu waliokuja kwenye show yake, utaweza kumuona
msanii Roma pamoja na Kala Jeremiah na Yusuph Mlela.
Mungu ailaze
roho ya marehemu Juma Kilowoko (Sajuki) mahala pema peponi, Amen.
No comments:
Post a Comment