Shomar Binda
Musoma
Taasisi
isiyo ya Kiserikali inayojishughulisha ya utoaji elimu katika Masuala mbalimbali katika Jamii,kuibua
changamoto na kusaidia Makundi yasiyojiweza ya Jamii Information Network (JIN) inatarajia kuendesha kongamano la vijana mjini Musoma mkoani Mara mwaka
huu wa 2013.
Akiongea na
waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Musoma,Mkurugenzi wa Taasisi hiyo
Augustine Mgendi amesema Kongamano hilo linatarajia kufanyika huku
likiwakutanisha Vijana zaidi ya 200 kutoka Shule 10 za Mjini hapa ambapo
linalenga kuwajengea stadi za kujitambua,kujiamini na kujithamini.
Alisema
katika Kongamano hilo vijana hao
watafundishwa kukabiliana na changamoto
zinazowakabili katika makuzi yao lakini pia kuhamasisha Vijana kupambana na Ugonjwa
wa Ukimwi,kujifunza mbinu za Ujasirimali,dhana ya kujiajiri na Changamoto
zake vijana kujenga
Uzalendo,kupambana na Umaskini,Rushwa
,Kuepuka Mimba za Utotoni katika Jamii.
‘Nadhani Vijana bado wanachangamoto kubwa
sana katika kufanikisha ndoto zao na hii ni fursa pekee kwa Vijana kujifunza
Mbinu mbalimbali maana tutakuwa na wataalam ambao wamebobea katika mambo hayo
ili kutoa Mwanga kwa Vijana wetu ” alisema Mkurugenzi huyo.
Mkurugenzi
huyo alisema kuwa Shule zitakazoshiriki Kongamano hilo zitatajwa baadaye baada
ya Mambo kadha wa kadha kukamilika
“Ni Shule kumi zitakazoshiriki na mambo
yakiwa tayari tutawafahamisaha ni shule gani ambazo tutakuwa nazo” alisema
Mkurugenzi huyo.
Mkurugenzi huyo alisema kuwa watakuwepo
wataalamu mbalimbali watakaohusika kutoa mafunzo katika Kongamano hilo huku
akisema kuwa Vijana ndiyo nguvu kubwa ya
Taifa kwasasa hivyo wanahitaj miongozo ya Kimaisha katika kujitambua.
Kongamano
hilo ambalo litakuwa linafanyika kila Mwaka litakuwa na kauli mbiu mbalimbali
ambapo alisema kwa Mwaka huu litakuwa na
Kauli mbiu ya “Jitambue Kijana” ambapo
alisema kuwa Kongamano hilo litawasaidia
Vijana wengi Kujitambua kutokana
na Changamoto zinazowakabili kwasasa.
“Tunatarajia Kongamano hili liwe linafanyika
kila Mwaka ili kutoa elimu na mwongozo
wa kimaisha kwa vijana na kwa kuanza mwaka huu kauli mbiu yetu
itafahamika kama Jitambue Kijana hii ni kutokana na vijana wengi kutofikia Malengo yako kutona na Changamoto
zilizopo”alisema Bw Mgendi.
Mbali na
Kongamano hilo taasisi ya Jamii Information Network ambayo hufanya shughuli zake mkoa wa Mara
inatarajia kutoa elimu mbalimba mkoani Mara ili jamii huska kwenda na wakati
kutokana asilimia kubwa ya Watanzania kuishi vijijini ambapo vyombo vya habari
kufika inakuwa tabu.
Aidha
Mkurugenzi huyo alisema kuwa Taasisi
hiyo inatarajia kutumia wanahabari mkoani Mara kuibua changamoto mbalimbali
zilizopo vijijini ili kuziweka bayana na kufanya vipindi mbalimbali kutoka
Vijijini ambavyo alisema vitaibua Changamoto zilizopo huko.
Katika
kufanikisha Kongamano hilo Mkurugenzi huyo ameyaomba Mashirika mbalimbali
kujitokeza kufadhili Kongamano hilo ambalo litakuwa ni msaada
mkubwa wa kuwajenga Vijana hasa mkoani
Mara.
“Mimi nayaomba mashirika mbalimbali kujitokeza
ili kufanikisha Kongamano hilo maana najua litakuwa msaada mkubwa sana kwa
Vijana ambapo kwa njia moja au nyingne
litaweza kubadili fikra za vijana wanapomaliza masomo yao’ alimalizia
Mkurugenzi huyo.
Nguvu kazi
ya taifa lolote duniani ni vijana,hivyo wasipoandaliwa vizuri leo,kesho
watakuwa bomu ambalo litakapolipuka litaangamiza taifa lote.Waafrika wanayo
methali isemayo “mtoto umleavyo ndivyo akuavyo”,hivyo kama tunahitaji kuwa na
kizazi bora chenye maadili,uzalendo na uwajibikaji tuanze kuwaandaa vijana sasa
kisaikolojia,kimaadili na kimtazamo.
Afisa Habari
na Uhamasishaji
Jamii
Information Network
No comments:
Post a Comment