Serikali wilayani Ngara mkoani Kagera imewapa siku 30 wafugaji kuondoka na ng’ombe wao kabla hatua za kuwasaka na kutaifisha mifugo yao hazijachukuliwa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, January 09, 2013

Serikali wilayani Ngara mkoani Kagera imewapa siku 30 wafugaji kuondoka na ng’ombe wao kabla hatua za kuwasaka na kutaifisha mifugo yao hazijachukuliwa.

Moja ya Kundi la  ng’ombe
Serikali  wilayani Ngara mkoani  Kagera imewapa siku 30 wafugaji wenye asili ya Rwanda kuondoka na ng’ombe wao kabla hatua za kuwasaka na kutaifisha mifugo yao hazijachukuliwa.

 

Mkuu wa Wilaya ya Ngara,Bw. Costantine Kanyasu ametoa agizo hilo pamoja na kupiga marufuku viongozi wa vijiji wilayani humo kuwapatia ardhi wahamiaji wenye mifugo kutoka ndani na nje ya  nchi.



Akizungumza na wafugaji wakubwa na wadogo wa Kata za Kasulo na Rusumo pamoja na viongozi wa kata hizo, Mkuu huyo wa wilaya amesema tamko hilo limetolewa baada ya kuwepo kwa baadhi ya wafugaji wenye asili ya Kinyarwanda na wengine kutoka wilaya za mikoa ya hapa nchini wanaoingia wilayani Ngara na ng’ombe wengi na kuwanyanyasa wazalendo wenye ng’ombe wachache.



Bw.Kanyasu amesema ili kuhakikisha amani na utulivu vinapatikana ndani ya siku 30, viongozi wa vijiji kwa kata zote wilayani Ngara wafanye usajili upya wa kuwatambua wafugaji wageni toka nje ya vijiji vyao na mifugo waliyo nayo na kubaini walioingia kihalali na walioingia kinyume, ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.



Amesema serikali inafanya kazi ya kulinda na kutetea haki za wananchi na sio kutetea kundi dogo lenye uwezo wa kifedha na kuwanyanyasa wachache, kwani kufanya hivyo ni kukiuka haki za binadamu na kukwepa uwajibikaji kwa mujibu wa sheria.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad