Mwandishi wa habari wa Radio Kwizera anayefanyia kazi wilayani Kakonko mkoani Kigoma Bw. Issa Ngumba amepotea katika mazingira ya kutatatisha ,Atakayemuona atoe taarifa Kituo chochote cha Polisi au Kwa Uongozi Uliokaribu nae. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, January 07, 2013

Mwandishi wa habari wa Radio Kwizera anayefanyia kazi wilayani Kakonko mkoani Kigoma Bw. Issa Ngumba amepotea katika mazingira ya kutatatisha ,Atakayemuona atoe taarifa Kituo chochote cha Polisi au Kwa Uongozi Uliokaribu nae.

Bw. Issa Ngumba.
Mwandishi wa habari wa Radio Kwizera anayefanyia kazi wilayani Kakonko mkoani Kigoma Bw. Issa Ngumba amepotea katika mazingira ya kutatatisha.


Taarifa kutoka Jeshi la Polisi wilayani Kakonko zinasema kuwa Bw Ngumba amepotea tangu January 05 mwaka huu majira ya saa 11 jioni ambapo alimuaga mke wake Bi. Rukia Yunus kuwa anakwendwa Muhange senta wilayani Kakonko na kwamba hajarudi nyumbani hadi sasa.



Kufuatia tukio hilo jeshi la polisi kwa kushirikiana na wananchi wa Kijiji cha Muhange wanaendelea kumtafuta katika mapori ya kijiji hicho baada ya rafiki zake kueleza kuwa aliwaanga kuwa anakwenda kutafuta dawa msituni.



Bw. Issa Ngumba.
Aidha jeshi la polisi Wilayani Kibondo limeomba kampuni za mitandao ya simu anayotumia Bw Ngumba kusaidia kutambua simu zake zilipotumika kwa mara ya mwisho ili kurahisisha upatikanaji wake.



Akizungumza kwa njia ya simu, Mke wa Bw Issa Ngumba, Bi Rukia Yunus amesema kuwa wananchi walio wengi ambao walikuwa wakimtafuta maporini wamerudi kijiji hapo baada ya kumkosa.


Habari:Radio Kwizera

2 comments:

  1. Ameshapatikana akiwa amekufa na mazishi ni leo tar 8 Jan 2013 - Tuapdatie usiwe mzee wa analojia.

    ReplyDelete
  2. Asante kwa hilo..tayari ndugu na ndo tumetoka mazikoni Kakonko na tunarudi Ngara.

    ReplyDelete

Post Bottom Ad