![]() |
Marehemu Issa Ngumba |
Akiongea baada ya Mazishi, Mwenyekiti wa Halmsahuri ya wilaya ya Kibondo Bw Juma Maganga amesema kifo cha Ngumba ni pigo kwa wilaya na taifa kwa ujumla.
Mkuu wa kituo cha Polisi Muhange OSC Alex Zakaria amesema Jeshi la Polisi
litahakikisha waliofanya mauaji ya Mwandishi huyo wa Habari wanakamatwa na wanafikishwa katika vyombo vya sheria.
Aidha
Mwili wa Issa Ngumba umeonekana leo (Januari 08,2013)majira ya saa tatu na nusu
Asubuhi karibu na mlima Kudyaluheta katika kijiji cha Muhange ukiwa umenyongwa.
![]() |
Marehemu Issa Ngumba |
Kwa
mujibu wa Dr Primus Ijuma wa Kituo cha Afya Kakonko aliyefanya uchunguzi wa
mwili huo amesema umeonyesha Bw Issa Ngumba ameuawa kwa kunyongwa na kisha
kupigwa risasi katika mkono wake wa kushoto.
Aidha
Simu na pesa alizokuwa nazo Bw Issa Ngumba hazikuchukuliwa lakini pia watu
waliofanya tukio hilo waliacha bastola karibu na mwili wake.
Awali
taarifa za Jeshi la Polisi zilisema kuwa Bw Ngumba alipotea tangu January 05
mwaka huu majira ya saa 11 jioni ambapo alimuaga mke wake Bi. Rukia Yunus kuwa
anakwendwa Muhange senta wilayani Kakonko na hakuonekana tena hadi alipokutwa
porini amefariki.
Katika Salamu
zake za rambi rambi Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Kigoma (KGPC)
kimeeleza kupokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha mwandishi huyo.
Mwenyekiti
wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Kigoma Bw Deogratius Nsokolo amelaani
mauaji hayo na kulitaka Jeshi la Polisi mkoani Kigoma kufanya uchunguzi wa kina
ili kubaini chanzo cha mauwaji hayo .
….
Mungu ailaze roho ya marehemu Issa
Ngumba…… mahala pema peponi, Amen.
No comments:
Post a Comment