Basi la Bunda lililokua linatokea Musoma kwenda Mwanza limepata ajali nje kidogo ya Magu eneo la katikati ya Kahangalala na Ihayabuyaga na watu watatu wanahofiwa kufariki katika ajali hiyo na zaidi ya 10 kujeruhiwa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, January 10, 2013

Basi la Bunda lililokua linatokea Musoma kwenda Mwanza limepata ajali nje kidogo ya Magu eneo la katikati ya Kahangalala na Ihayabuyaga na watu watatu wanahofiwa kufariki katika ajali hiyo na zaidi ya 10 kujeruhiwa.


Basi la Bunda lililokua linatokea Musoma kwenda Mwanza limepata ajali nje kidogo ya Magu eneo la katikati ya Kahangalala na Ihayabuyaga na watu watatu wanahofiwa kufariki katika ajali hiyo na zaidi ya 10 kujeruhiwa.


Mazingira yanaonesha kuwa idadi kubwa ya watu wamejeruhiwa na hofu kubwa imetanda eneo la tukio kuhofia usalama wa hali za abiria waliomo ndani ya basi husika kwani basi limepinduka tairi zikielekea juu, limetumbukia kwenye majaruba ya mpunga, limepondeka vibaya upande mmoja.

Hakuna pa kujisitiri kwa watoto hawa ambao walikuwa wakisubiri wazazi wao kuokolewa toka ndani ya basi hilo zaidi ya kujisitiri kwa kanga, vitenge na mashuka waliyoambulia toka kwenye baadhi ya mabegi yao.

Hali ya baadhi ya barabara za ndani zinazounganisha vijiji wilayani Magu zimefunikwa na maji na hii ndio Barabara na hali ya hewa na mazingira.

Baadhi ya nyumba zilizo karibu na eneo la ajali nazo zimeathiriwa na mvua kubwa inayoendelea kunyesha eneo hili wilayani Magu.

Hali ya uokoaji imeathiriwa na mvua kubwa inayoendelea kunyesha eneo hili ni wachache tu abiria wameweza kupewa miamvuli na watu walio kwenye magari yanayopita eneo hili ili wapate kujisitiri.




PICHA KWA HISANI YA GSENGO

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad