Wezi warudisha vifaa vya Sharomilionea kwa kuvisalimisha usiku na wengine wanavileta mchana kwa mwenyekiti wao. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 03, 2012

Wezi warudisha vifaa vya Sharomilionea kwa kuvisalimisha usiku na wengine wanavileta mchana kwa mwenyekiti wao.

Tairi la gari
Jeshi la Polisi mkoani Tanga limefanikiwa kukamata vitu mbalimbali vya marehemu Hussein Ramadhan, ‘Sharo Milionea’ vilivyoibwa na watu wasiojulikana, muda mfupi baada ya msanii huyo wa filamu na muziki nchini kupata ajali katika Kijiji cha Songa Kibaoni, wilayani Muheza na kufariki dunia papo hapo.




Akizungumza na waandishi wa habari , Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Costantine Massawe alisema Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata begi la nguo, simu ya mkononi aina ya blackberry, betri ya gari, redio, tairi la gari na saa ya mkononi ya marehemu.



Alitaja vitu vingine vilivyopatikana kuwa ni nguo ambazo marehemu alivuliwa baada ya kupata ajali, ambazo ni fulana na suruali ya jeans.



Alisema kuwa,vitu hivyo vilipatikana baada ya wakazi wa kijiji ilipotokea ajali hiyo kuvisalimisha vitu hivyo kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Songa kibaoni, Abdi Zawadi ambaye alitoa taarifa polisi kwa ajili ya utambuzi na taratibu nyingine,” .



Begi la nguo, simu ya mkononi aina ya blackberry, betri ya gari, redio



Kamanda Massawe alisema baadhi ya vitu hivyo vilikamatwa nje ya wilaya ya Muheza katika gereji na kwenye nyumba za watu.



Kamanda alifahamisha zaidi kuwa, hadi sasa watu kadhaa wanashikiliwa na jeshi hilo kwa kuhusika na tukio hilo lakini hakutaja idadi yao kwa kuwa vitu vingine havijapatikana.




Gari aliyokuwa akiendesha Marehemu Sharomilionea baada ya kuacha njia na kupinduka 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad