Kilimanjaro Stars na Zanziba Heros hao watinga kiume Nusu Fainali ya Kombe la CECAFA Tusker Challenge sasa kwasubili washindi kati ya Uganda v Ethiopia na Kenya v Malawi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 03, 2012

Kilimanjaro Stars na Zanziba Heros hao watinga kiume Nusu Fainali ya Kombe la CECAFA Tusker Challenge sasa kwasubili washindi kati ya Uganda v Ethiopia na Kenya v Malawi.

Fans wa  Kilimanjaro Stars
Timu ya Tanzania  Bara imefanikiwa kuingia Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki  na Kati, CECAFA Tusker Challenge baada ya kuilaza Timu ya Rwanda mabao 2 - 0 kwenye  Uwanja  wa Lugogo mjini Kampala Uganda.




 Hadi mapumziko Kilimanjaro  Stars walikuwa mbele kwa bao 1 - 0 lililotiwa kimiani na kiungo Amri Kiemba, dakika mya 33 akiunganisha pasi ya Mwinyi Kazimoto aliyewapunguza wachezaji wawili wa Rwanda kabla ya kutoa pasi maridadi.



Kipindi cha pili  Kilimanjaro Stars walirudi vizuri tena na kuendelea kucheza kwa kuonana na kufanikiwa kupata bao la pili 53 baada ya John Bocco kuuwahi mpira uliotemwa na kipa Jean Claude Ndoli kufuatia shuti kali la Mwinyi Kazimoto kutoka nje ya eneo la hatari.



Kwa ushindi huo  Kilimanjaro Stars  sasa inasubiri mshindi kati ya Uganda na Ethiopia kesho watakapo kutana naye kwenye  hatua ya Nusu Fainali.



Mshambuliaji wa timu ya Kilimanjaro Stars inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Mrisho Ngasa aliyelala chini na wachezaji wenzake wakishangilia kwa staili ya aina yake baada ya kuwafunga Rwanda 2-0 katika mchezo wa Robo Fainali ya kwanza ya michuano ya Cecafa Challenge uliochezwa katika Uwanja wa KCC uliopo Lugogo nchini Uganda


Zanziba Heros
Nao Zanziba Heros   imeingia  hatua ya Nusu Fainali ya Kombe  hilo la CECAFA Tusker Challenge baada ya kuifunga Burundi kwa penalti 5 - 4 kwenye Uwanja huo huo wa Lugogo  mjini Kampala, Uganda  kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90. 



Kwa matokeo hayo, Zanzibar sasa itacheza na mshindi kati ya Kenya na Malawi katika Nusu Fainali.



Shujaa wa Zanzibar  alikuwa ni Abdallah Othman aliyefunga penalti ya mwisho, baada ya kipa Mwadini Ally kupangua penalti ya Abdul Fiston wa Burundi.



Aidha manahodha wa timu zote, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wa Zanzibar na Suleiman Ndikumana wa Burundin walipoteza penalti zao leo.




Kikosi cha Zanzibar Heroes kilichopambana na Burundi katika mchezo wa Robo Fainali ya Pili ya michuano ya Cecafa Challenge uliochezwa katika Uwanja wa KCC uliopo Lugogo nchini Uganda.


Kili  Stars: Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Amir Maftah, Shomary Kapombe, Kevin Yondan, Amri Kiemba, Salum Abubakar/Athumani Iddi dk51, Frank Domayo, Mwinyi Kazimoto, Mrisho Ngassa na John Bocco/Shaaban Nditi dk 85.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad