Wakazi 6 wa kijiji cha Mugoma wilayani Ngara mkoani Kagera , wamefikishwa Mahakama ya wilaya hiyo, wakishitakiwa kwa mauaji ya Askari wawili na kuchoma moto kituo cha Polisi Mugoma. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, December 21, 2012

Wakazi 6 wa kijiji cha Mugoma wilayani Ngara mkoani Kagera , wamefikishwa Mahakama ya wilaya hiyo, wakishitakiwa kwa mauaji ya Askari wawili na kuchoma moto kituo cha Polisi Mugoma.


Kituo cha Polisi kata ya Mugoma
wilayani Ngara mkoani Kagera
kikiwa kimechomwa moto.

Wakazi sita wa kijiji cha Mugoma wilayani Ngara, leo(Desemba 21,2012)  wamefikishwa katika Mahakama ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera  wakishitakiwa kwa mauaji ya Askari wawili na kuchoma moto kituo cha Polisi kata ya Mugoma wilayani humo.



Waendesha mashitaka wa Jeshi la Polisi Hamisa Mataka na Tumaini Membi, wamewataja washitakiwa kuwa ni Method John  ambaye ni afisa Mtendaji wa kijiji cha Mugoma, Suleimu Zuberi, Rashid Ally, Issa Athumani, Simon Chuma na Aman Maulid.



Amesema watu hao wanatuhumiwa kuwaua Koplo Paschal na Konstebo Alexandar, ambao walikuwa waajiriwa wa jeshi la polisi Tanzania, katika tukio lililotokea Desemba 15 mwaka huu majira ya saa 8 mchana, katika eneo la Mugoma.



Katika shitaka la pili, watu hao wanashitakiwa kwa kosa la kuchoma moto kituo cha polisi cha Mugoma, na kusababisha hasara yenye thamani ya zaidi shilingi milioni 68, kutokana na uharibifu wa mali mbalimbali za jeshi hilo.



Washitakiwa hawakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa walikuwa mbele ya mlinzi wa Amani Bw. Andrew Kabuka, na pia mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi za mauaji, ambapo wamerudishwa rumande hadi January 3 mwaka kesho.




Chanzo:Radio Kwizera FM.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad