Wakati Mamia ya wakazi wa wilayani Ngara mkoani Kagera wakishiriki maziko ya mkazi wa kijiji cha Mugoma aliyeuawa kwa kupigwa risasi na Polisi ,Jeshi la Polisi limesema nchi inaongozwa na utawala wa sheria hivyo serikali haitakubali watu kujichukulia sheria. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 17, 2012

Wakati Mamia ya wakazi wa wilayani Ngara mkoani Kagera wakishiriki maziko ya mkazi wa kijiji cha Mugoma aliyeuawa kwa kupigwa risasi na Polisi ,Jeshi la Polisi limesema nchi inaongozwa na utawala wa sheria hivyo serikali haitakubali watu kujichukulia sheria.


Kituo cha police Mugoma wilayani Ngara



mkoani Kagera kikiwa kimechomwa



moto na wananchi,baada



ya asikari police kumuua



mkazi mmoja kwa risasi



na hivyo kusababisha vurugu



zilizopelekea askari



wawili kufariki dunia.
Mamia ya wakazi wa wilayani Ngara jana(Desemba 16,2012) wameshiriki maziko ya mkazi wa wa kijiji cha Mugoma wilayani Ngara mkoani KAGERA aliyeuawa, kwa kupigwa risasi na Polisi hali iliyosababisha Askari wawili nao kuuawa na wananchi wenye hasira ambao pia walichoma moto Kituo cha Polisi  Mugoma.

 

Akiongea na wananchi katika msiba huo Kamanda wa Polisi mkoani Kagera Bw Philip Kalangi amesema nchi inaongozwa na utawala wa sheria hivyo Serikali haitakubali watu kujichukulia sheria.



Amesema Polisi wanajukumu la kulinda usalama wa raia na mali zao na kwamba polisi na raia watakaobainika kuhusika na tukio hilo watachukuliwa hatua stahiki.



Mwananchi aliyeuawa na Polisi na kuzikwa jana ni Said Nkonikoni mkazi wa Mugoma na askari Polisi waliouawa na wananchi wenye hasira, Koplo Pascal na Konstebo Alex wa Kikosi cha Usalama Barabarani ambao miili yao imeagwa jana na kupelekwa mikoa ya Mwanza na Morogoro kwa maziko.


Habari:Radio Kwizera/www.radiokwizera.com

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad