Waziri wa
Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi akisoma hotuba yake.
|
Baadhi
ya Kinamama
na
watoto wao waliojitokeza
katika
uzinduzi wa Chanjo hizo.
|
Tanzania kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii leo imezindua chanjo mpya zinazolenga kukinga watoto dhidi ya nimonia na magonjwa ya kuhara yanayo sababishwa na kirusi cha Rotavirus.
Akizindua
chanjo hiyo leo Mke wa rais Mama Salma Kikwete amesema kirusi cha Rotavirus
kinachangia asilimia 18 ya vifo vya watoto vinavyotokana na kuharisha.
Amesema
kuongezeka kwa chanjo hizi hapa nchini kutapunguza vifo vya watoto vitokanavyo
na maradhi haya ili kufikia lengo la mileni namba 4 ifikapo 2015.
Aidha Mama
Salma ametoa rai kwa wananchi kuendeleza juhudi mbalimbali za kuboresha afya
ikiwa ni pamoja na kunawa mikono kwa nyakati muhimu hususan kabla ya kula au
kuandaa chakula, pia baada ya kujisaidia.
Mama Salma
Kikwete akitoa chanjo kwa mmoja wa watoto kuashiria uzinduzi wa chanjo mpya za
“PVC 13 na Rotarix” kukinga watoto dhidi ya Nimonia na magonjwa ya kuhara.
|
No comments:
Post a Comment