Rais Jacob Zuma |
Bw. Zuma
ameshinda kwa karibu
kura 3,000, wakati Makamu wake
aliyekuwa pia akiwania nafasi hiyo Kgalema Montlante amepata kura
chini ya 1,000
katika uchaguzi wa uongozi
wa chama hicho
uliofanyika leo.
Upigaji kura
ulianza asubuhi ya leo katika
mkutano wa ANC wa
Mangaung, uliofanyika katika mji
ambao pia unafahamika kama
Bloemfontein.
Takriban
wajumbe 4,000 wamepiga
kura katika kinyang’anyiro hicho
cha uongozi wa
juu wa chama cha
ANC.
Bwana Motlanthe sasa amepoteza nafasi yake ya naibu kiongozi wa chama hicho na mahala pake pamechukuliwa na mfanyabiashara maarufu na mwanaharakati dhidi ya ubaguzi wa rangi Cyril Ramaphosa, ambaye sasa atakuwa makamu wa rais wa Afrika Kusini. Mshindi wa nafasi hiyo ndiye atakayekuwa na nafasi ya kushinda uchaguzi wa mwaka 2014.
Wajumbe wa
chama cha ANC
|
Bwana Motlanthe sasa amepoteza nafasi yake ya naibu kiongozi wa chama hicho na mahala pake pamechukuliwa na mfanyabiashara maarufu na mwanaharakati dhidi ya ubaguzi wa rangi Cyril Ramaphosa, ambaye sasa atakuwa makamu wa rais wa Afrika Kusini. Mshindi wa nafasi hiyo ndiye atakayekuwa na nafasi ya kushinda uchaguzi wa mwaka 2014.
Chama cha
ANC kimeshika hatamu nchini Africa Kusini tangu kumalizika kwa utawala wa
ubaguzi wa rangi mwaka 1994.
Polisi
nchini humo, hapo jana waliwatia mbaroni watu wanne baada ya taarifa kuzagaa
kwamba walikuwa na mpango wa kulipuwa ukumbi unaotumiwa na wajumbe hao wa chama
cha ANC.
Baada ya
uchaguzi huo kucheleweshwa kwa masaa kadhaa, zoezi la kupiga kura lilianza saa
sita usiku na kukamilika majira ya saa moja asubuhi kwa saa za Afrika Kusini.
Wajumbe hao
walioonekana wamechoka huku wakijifunika mablanketi walionyesha vidole vyao
vikiwa na alama ya wino.
Wajumbe hao
wamekuwa wakipiga kura kwa ajili ya nafasi ya uongozi wa juu wa chama hicho.
Rais Zuma |
Wafuasi wa
rais Zuma, tayari wanaendelea kusheherekea, kufuatia ushindi huo mkubwa.
Rais Zuma
analaumiwa kwa kushindwa kupunguza umaskini au kutatua tatizo la ufisadi ndani
ya chama cha ANC na serikali, wakati mwezi wa nane mwaka huu watu walishangazwa
na jinsi polisi walivyowapiga risasi na kuwauwa wachimba madini 34 ambao
walikuwa wamegoma.
No comments:
Post a Comment